BREAKING NEWS-MAHAKAMA KUU YAMPUNGUZIA ADHABU MRAMBA NA YONA,NI BAADA YA RUFAA YAO,SOMA H
NA KAROLI VINSENT
HATIMAYE mahakama Kuu imewapunguzia adhabu mawaziri wa wa awamu ya tatu
ambao ni Waziri wa fedha Basil Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini
wa serikali ya awamu ya Tatu Daniel Yona toka miaka mitatu jera waliohukumiwa mwanzo, hadi miaka miwili.
Hukumu hiyo imefuata
baada mahakama hiyo chini Hakimu Protas Rugazia kutupilia mbali rufaa iliyotaka
washitakiwa hao kuachiwa huru na badala yake wamepunguziwa adhabu kutoka hukumu
ya miaka 3 na fidia ya shilingi milioni 5 katika mahakama ya mkaazi Kisutu ambapo sasa wote kwa pamoja wanatakiwa kwenda jera miaka miwili kila mmoja.
![](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_sIiu4gKJORtxAfFvPhxHR5ENqOtT9YGC8XChKNlwlBFViiNJex9uiZnJOLyTw5tvYc8MG1vI82SfqAu46YBNY7A6Hv14gs1MR1yiUNvbiMIrORfptYHLUTrTdnrWMXxXhRrSkYloc=s0-d)
Aidha Hakimu Rugazia amesema hatua ya
kuwapunguzia adhabu imefuata baada ya kujiridhisha kuwa adhabu iliyokuwa
imetolewa mwanzoni haikulingalina na uzito wa kosa walilotenda.
Mpaka mtandao
huu unaondoka mahakamani hapo mawakili
upande wa washitakiwa hao hawakuwa tayari kuizungumzia hukumu hiyo
Bazir Mramba na mwenzake Daniel Yona walikuwa wanatuhumiwa kwa kosa la matumizi mabaya ofisi ya umma ambapo waliisababibishia serikali hasara ya shilingi Bilioni 11.7.
Bazir Mramba na mwenzake Daniel Yona walikuwa wanatuhumiwa kwa kosa la matumizi mabaya ofisi ya umma ambapo waliisababibishia serikali hasara ya shilingi Bilioni 11.7.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni