Zinazobamba

LOWASSA NA MAGUFULI WAMTISHA MKURUGENZI WA TANESCO ATANGAZA KUMALIZA MGAO WA UMEME NCHI NZIMA,SOMA HAPO KUJUA

Mkurugenzi wa shirika la ugavi wa umeme nchini TANESCO Felchesmi Mramba.
Mkurugenzi wa shirika la ugavi wa umeme nchini TANESCO Felchesmi Mramba

NA KAROLI VINSENT
SIKU moja kupita baada ya wagombea wa Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema ambaye anaungwa mkono na vyama vya UKAWA Edward lowassa pamoja na Mgombea Urais kupia CCM John Magufuli,
 kumtishia kumfukuza kazi mkurugenzi wa shirika Shirika la umeme nchini TANESCO endapo moja wao akiingia madarakani, kwasababu ya mgao wa umeme unaoendeleo nchini
Hatimaye sasa Mkurugenzi huyo wa  TANESCO ameibuka na kuwahakikishia watazania kuwatatizo la kukatika kwa umeme litakuwa limekwisha ndani ya wiki hii,   na kurejesha umeme katika hali yake ya  kawaida.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam  mkurugenzi wa tanesco Felchesmi Mramba  amesema mpaka jana wamefanikiwa kuwasha  mtambo wenye megawati  35 unaomilikiwa na kampuni ya Symbion,ambao kwa kiasi kikubwa umeongeza  nguvu katika gridi ya taifa na  baadhi ya maeneo yamekuwa yakipata umeme wa uhakika.
Aidha  amesema Tanesco inafahamu hali ngumu ya kukatika kwa  umeme wanayo kumbana nayo wananchi katika mikoa ya arusha,Mwanza,Kilimanjaro,Mbeya,Dodoma,na kwingineko ambapo amewaomba radhi wananchi na kuwataka  waendelee kuwa na subira wakati shirika hilo likiendelea kurekebisha hali hiyo.
Pia amefafanua kuwa hali katika  mabwawa ya kuzalishia umeme wa maji sio nzuri mara baada ya kupungua kwa asilimia  81.3 na hivyo husababisha ukosefu wa umeme.
Mkurugenzi huyo  ameeleza kupatikana kwa umeme wa gesi kutaendelea  kukuza na kuboresha hali ya umeme nchini  na kusisitiza Tanesco itaendelea kutoa taarifa kila wiki  ili kuwapa wananchi  taarifa jinsi  hali inavyoendelea .
Hata hivyo amesema shirika hilo ndani ya wiki hii  linatarajia kupata kiasi kingine cha umeme ambapo  megawati 70 kutoka   Kinyerezi megawati 20 kutoka Syimbion.


Hakuna maoni