KUMEKUCHA SASA-WAISLAM WAJILIPUA SASA,WAMTANGAZIA KIAMA KIKWETE NA SERIKALI YAKE,MZIMU WA SHEHE PONDA WAIBUKA SOMA HAPA KUJUA
| Pichani ni Mwenyekiti Jumuiya ya Taasis ya Kiislam Sheikh Mussa Kundesha Akizungumza na Wanahabari leo Jijini dar es Salaa awapo Pichani |
JUMUIYA na
Taasis ya Kiislma nchini (T) imempa siku 15 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Ernest Mangu,kuwaachia mara moja Viongozi wa Dini ya Kiislam waliokamatwa kama
makosa mbali mbali la Sivyo Jumuiya hiyo itaitisha maandamano nchi nzima
kupinga wanachodai ni uonevu wanaonewa na Serikali.Anaandika KAROLI VINSENT
endelea nayo
Kauli hiyo imetolewa Leo Jijini Dar es
Salaam na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo
ambayo ni muunganiko wa Taasisi 11 za dini ya kiislam nchini Sheikh Mussa Kundesha
Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema Wameshoka na kile wanachodai ni kuonewa na
Jeshi la Polisi kitendo cha kuvamia Misikiti mbali mbali nchini na
kuwabambikizia Mashehe Kesi za Ugaidi na kushindwa kuwapa Dhamana.
“Tumempa
siku 15,mkuu wa Jeshi la Polisi nchini awe amewaanchi mara moja viongozi wetu wa dini yetu waliokamatwa kwa
kesi zisizo kuwa na kichwa na miguu,lasivyo akikaidi tutaitisha maandamo ya
Amani kupinga uonevu huu”amesema Sheikh Kundesha.
Shekh Kundesha ameongeza kuwa mbali na Jeshi la Polisi kuwakamata viongozi hao
,Lakini jeshi hilo limeshindwa kuwaachia kwa Dhamana viongozi hao, wakati
huo huo amesema Jeshi hilo likiwaachia kwa Dhamana Maaskofu wanaotoa lugha za
kichochezi ikiwamo Askofu Josephat Gwajima.
“Huu ni uonevu gani tunafanyiwa na
Serikali kwani Sheikh Ponda kwa sasa ni miaka miwili yupo ndani sio kwasababu
ya Amri ya Mahakama bali ni ya Amri ya muendesha Mashtaka DPP eti kwa kutoa
maneno ya kichochezi lakini kesi hiyo hiyo anayesema ni ya Uchochezi inaendana
na Askofu Gwajima pamoja Viongozi wengine wa Dini ya Kikristo ,lakini wako huru
vipi Shehe Ponda”Amehoji Sheikh Kundesha.
Aidha,Sheikh Kundesha huku akiongea kwa
Uchungu amesema kwa sasa Jumuiya hiyo imesikitishwa na kitendo anachokiita ni
cha kuizika Dini ya Kiislam nchini kwa Jeshi la Polisi kuendeleza kuwakamata Walimu
wanaofundisha watoto wa Dini ya hiyo kwenye Madrasa na kuwapa kesi mbali
mbali.
“Kule moshi mkoani Kilimanjaro watoto na
Walimu wa Madrasa wamekamatwa kama ilivyokuwa Mkoani Mtwala Mwalimu wa Madrasa
bado wanashikiliwa na Polisi kwa kuwa na watoto wanawafundisha Dini ya
Kiislam “
“Dodoma watoto wa tatu wa madrasa,Walimu
wao na mwenye Nyumba wanakowafundisha watoto dini ya Kiislam waliwakamata na
kupelekwa kituo cha polisi kuhojiwa na kuchukuliwa kama wahalifu wengine hivi
nia ya serikali ni ipi”ameendelea kuhoji.
Pamoja na hayo amebainisha kuwa kwa sasa
Walimu ambao walikuwa wanafundisha madrasa wametangaza kuachana na kazi hiyo ya
kuwapa Elimu watoto wa Kiislam kwa kitendo cha Jeshi la Polisi kuwakamata na
kuwapa kesi ya mbalimbali,
Vilevile Sheikh huyo awataka waislam
kujitokeza mnamo tarehe 15/05/2015 kwenye Maandamano hayo ya Amani kwa lengo la
kupaza Sauti zao ili Dunia isikia mateso wanayoyapata Waislam wenzao nchini.
No comments
Post a Comment