Zinazobamba

BREAKING NEWS-MABASI YA MIJINI KUGOMA TENA JUMATATU NCHI NZIMA,MADEREVA WAAPA KUTUMUOGOPA MTU,SOMA HAPA KUJUA

Katibu Mkuu wa Chama cha Madareva Tanzania (TTDA), Rashid Sahel
Katibu Mkuu wa Chama cha Madareva Tanzania (TTDA),
Rashid Sahele

 akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) PICHA NA MAKTABA
NA KAROLI VINSENT
SIKU moja kupita baada ya Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta kufanikisha kutuliza Mgomo uliokuwa unataka kufanywa na Wamiliki wa Magari yaendayo Mikoani (TABOA)kupinga tozo za Nauli mpya,Baada ya Waziri huyo kufutilia mbali Nauli hiyo mpya iliyotangazwa na Mamlaka ya Usafiri wa Nchi kavu na Majini (SUMATRA).
   Nao pia UMOJA wa Madereva Tanzania (TTDA) umetangaza mgomo wa Mabasi wa yanayofanya kazi ya kupakia Abiria mijini nchi nzima kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo kwa madai ya Serikali kupuuza matakwa yao
          Akitangaza Mgomo huo, mda huu,Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa TTDA, Rashid Salehe   wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema kitendo cha Waziri wa Kazi na Ajira  Gaudentia Kabaka kupuuza matakwa ya kuonana nao ili wamwelieza madai yao wanayoadai kwa mda mrefu
     Katibu huyo aliyataja Madai hayo ni Kupatiwa Mikataba ya Ajira ya kulipwa kila mwezi ambapo kwa sasa hawana na Kuanza kulipwa kwa utaratibu wa Kilomteka kwa saa pamoja na kuwekewa pesa kwenye mifuko ya hifadhi ya Jamii iwadaidie pindi wanapopata Ajali na ikwemo wakati uzeeni .
        Dereva Salehe ameongeza kuwa uamuzi wa kugoma  kuendesha Mabasi itakuwa chachu ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kusikiliza kilio chao cha Mda mrefu ambacho wanasema Waziri mwenye dhamana ya Kazi kuyapuuza.

          Pamoja na hayo amebainisha kuwa kwa sasa wameshawataarifu Madereva wote nchi nzima kutoendesha Mabasi kuanzia Jumatatu ya wiki Ijayo mpaka pale Mmlaka husika itakaposikia Kilio chao cha kuwahamulu wamikiliki wa Mabasi kuwatekelezea madai hayo.

No comments