HABARI ILIYOTIKISA JIJI.UKAWA WAMALIZANA,WAMTISHWA GUNIA LA MISUMARI KIKWETE,SOMA HAPA KUJUA
| Viongozi wakuu wa vyama vikuu vya upinzani UKAWA wakiwasili makao makuu ya CUF kwa ajili ya kuzungumza na wanahabari leo |
HATIMAYE
viongozi wa Vyama vikuu vya Upizanzani nchini vinavyounda (UKAWA) vimeibuka na kufichua mipango ambayo wanadai inatakakufanywa na Chama cha
Mapinduzi CCM na kushirikiana na Tume ya Uchaguzi nchini kumwongezea mda Rais
Jakaya Kikwete kwa miaka miwili.
Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
Vilevile pia Viongozi hao wametangaza
rasmi ya kwamba kutokuwa na Imani na
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwakusema inataka kumlinda Rais Kikwete abaki
Madarakani kwa kuharibu uandikishaji wa Wapiga kura kwa Mfumo wa Mpya wa BVR.
Kauli hizo za UKAWA ambao ni Muunganiko
wa Vyama vya siasa nchini ambavyo ni CHADEMA,CUF,NCCR-Mageuzi pamoja na NLD
imetolewa mda huu Jijini Dar es Salaam
Wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika Kikao cha
Siku mbili kilichowakutanisha Viongozi hao, kujadili masuala mbali mbali kuelekea
kwenye uchaguzi Mkuu hapo baadae-
Ambapo Akisoma
Tamko hilo la UKAWA kwa niaba ya Viongozi wenzake,Mwenyekiti wa Chama
cha NCCR-Mageuzi James Mbatia ambapo- amesema kuwa kutokana na hali ya hewa
inayoendelea kuhusu sintofahamu ya daftari la kupiga kura ni wazi kuwa sasa
umoja wao hauna inami hata kidogo na tume ya uchaguzi kwani imeonyesha wazi
kuwa inashirikiana na serikali ya chama cha mapinduzi kutaka kuhujumu uchaguzi
ujao na kisha kuongeza muda wa uongozi wa serikali hiyo kwa kisingizio cha
kutokumalizika kwa uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.
Amesema kuwa tume ya taifa ya uchaguzi
hadi sasa ikiwa imesalia takribani miezi mitatu pekee kuanza kwa kampeni rasmi
za uchaguzi haijaanza wala hakuna dalili za maandalizi yoyote ya kufanyika kwa
uchaguzi huo jambo ambalo linazidi kuleta wasiwasi kwa watanzania na kuamini
kuwa kuna njama za kuahirisha uchaguzi huo kama ilivyofanyika kwa daftari la
kudumu la wapiga kura.
| WANAHABARI WAKIWASIKILIZA VIONGOZI WA UKAWA |
“kuna jambo linashangaza sana,hadi
sasa hakuna maandalizi yoyote yanayoashiria kuwepo kwa uchaguzi huo ilihali
imebaki miezi sita tu kufanyika kwa uchaguzi huo,hakuna utaratibu wa vifaa vya
uchaguzi huo,ambapo miaka iliyopita imekuwa ikifanyika maadalizi mwaka mmoja
kabla lakini uchaguzi huu hadi leo hakuna maandalizi ya kuonyesha kuwa uchaguzi
huo upo japo kuwa mwenyekiti wa tume hiyo anazidi kuwdanganya watanzania kuwa
uchaguzi huo upo”.aliseama mh MBATIA.
Naye mwenyekiti wa CHADEMA mh FREMAN
MBOWE amesema kuwa hakuna njia yoyote ya kuzia mabadiliko ambayo yanataka
kufanywa na ukawa kwa sasa hivyo tume hiyo isikubali kutumika na serikali na
badala yake ni lazima uchaguzi ufanyike mwaka huu kwa njiia yoyote.
MGOGORO KUHUSU MAJIMBO
Wakati huo huo
UKAWA umetangaza rasmi mchakato wao wa kugawana majimbo ambapo
mwenyeikiti mwenza wa umoja huo mh MBATIA amesema kuwa hadi sasa mchakato huo
unaendelea viruzi ambapo majimbo 227 sawa na asilimia 95 ya majimbo
yote Tanzania yameshapata wagombea huku majimbo 12 yakiwa yamesalia huku
akisema kuwa ni maridhiano ndio yanaendelea na hakuna mgogoro kama
inavyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Akizngumzia habari ambazo
jana zilienezwa na baadhi ya magazeti nchini zikimtaja mwenyekiti wa NCCR
mageuzi mh JAMES MBATIA kuandika barua ya kujiondoa katika umoja huo kwa kile
kilichotajwa kuwa ni kutoridhika na mchakato wa ugawanaji wa majimbo
hayo,MBATIA amesema kuwa UKAWA walisikitishwa sana na taarifa hizo za upotoshaji
jambo ambalo amesema kuwa ni uzushi ambapo amesema kuwa taarifa hizo zina lengo
la kuhujumu umoja huo na kuipa nafasi CCM jambo ambalo halitakubalika katika
kipindi hiki ambacho watanzania wanahitaji mabadiliko.
Akizungumzaia taarifa hizo mwenyekiti
wa chadema mh MBOWE amesema kuwa huu ni wakati ambao mambo mengi sana yataibuka
ya kuzusha ili kuwagombanisha lakini wapo tayari kupambana na taarifa hizo na
hakuna wa kuwagombanisha.
| pichani ni mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe |
“Hakuna wa kuwatenganisha UKAWA kwa
sasa,najua tunawindwa sana na watu ili tugombane ili watu wapate cha
kusema,nasema hivi hakuna kitu kama hicho na hakivunjiki kitu hapa tupo imara
na tupo GADO kupambana hadi dakika ya mwisho”,amesema Mh MBOWE.
Akizungumzia mchakato wa kumpata
mgombea urais kupitia umoja huo mwenyekiti wa chama cha NLD mh DK EMANUEL
MAKAID amesema kuwa watanzania watulie kwani mgombea tayari ameshapatikana na
muda wa kumtaja ukifika watamtaja lakini sasa ibaki kuwa siri kwani kuna baadhi
ya vyama bado hata havina mtu wa kumsimamisha katika nafasi hiyo ya urais.
No comments
Post a Comment