Zinazobamba

SERIKALI YAIPIGIA DEBE KATIBA PENDEKEZWA,WAZIRI SAMIA SEMA HAYA,SOMA HAPA KUJUA



SERIKALI nchini imeendelea kuipigia debe Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba kwa kusema Katiba hiyo ni itakuwa ni mwarubaini wa kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuwataka wananchi waipigire kura ya ndio pindi itakapofika kwao.Anaandika KAROLI VINSENT endela nayo
         Kauli hiyo ya Serikali imetolewa leo tarehe 23 mwezi wa nne mwaka 2015, Jijini Dar es Salaam na Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu Hassan (Pichani)Wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari ambapo amesema katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum itakuwa mwarubaini wa matatizo ya muungano kutokana na katiba hiyo kutatua changomoto ambazo zimekuwa zikipigiwa kelele     siku nyingi.
          Waziri Samia amezitaja Changamoto ambazo adai katiba hiyo imezitatua ni Suala la mfumo wa Elimu kwenye Vyuo vikuu,haki ya kumilikia Ardhi upande wa bara,Rasimali ya mafuta na gesi pamoja na uwiano wa kulipa Deni la Taifa liliopo sasa .
       Bi Samia anasema licha ya Katiba mpya kuja njia ya kutatua  changomoto hizo pia anasema kwenye katiba hiyo kuna mambo mengi muhimu yamewekwa kwenye Katiba hiyo na yanayohusu muungano jambo ambalo anadai litaleta maendeleo katika nchini.

         Pamoja na hayo Waziri Samia ameendelea kuwataka watanzania kuisoma Katiba pendekezwa na kuipigia kura ya ndio katiba hiyo pindi itakapokuja kwao.

No comments