Zinazobamba

HABARI KUBWA.WAZIRI WASIRA AWATIMUA VIGOGO,NI WA MAMLAKA YA RUBADA,WAMEIBA BILIONI 2.5,WAJILIPA POSHO HOVYO HOVYO SOMA HAPA KUJUA

   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.

WAZIRI wa kilimo, Chakula na Ushirika Steven Wasira (pichani)amewafukuza Kazi wakurugenzi watendaji wa   Mamlaka ya Kuendeleza Bonde la Mto Rufiji (Yaani Rufiji River Basin Development Authority – RUBADA) kutokana na matumizi mabaya ya ofisi ya Umma ambayo yameitia  hasara Serikali  zaidi ya Bilioni 2.5.Aripoti KAROLI VINSENT endelea nayo.
          Wakurugenzi hao walifukuzwa ni Kaimu mkurugenzi wa shirika hilo Bwana Alocy Masanja wengine ni mkurugenzi wa Fedha Bwana Filozi John Mayayi     pamoja na Mkurugenzi wa Mipango wa shirika hilo Bibi Tabu Ndatulu   .
        Waziri Wasira ametangaza uamuzi huo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Vyombo mbalimbali vya Habari ambapo amesema  baada ya Ofisi yake kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wa  vijiji vya Rufiji pamoja na wawekezaji juu ya Urasimu wa shirika hilo  ikiwemo kuchukua fedha na kutowapatia Viwanja ndipo akaunda timu ya Uchunguzi kutoka wizara ya Kilimo na Hazina kwenda kuchunguza malalamiko hayo.
        “Baada ya kuunda tume ofisini kutoka hapa Wizarani na kushirikiana na Hazina kwenda kwenye Mamlaka ya Rubada kupitia hati ya za risiti,tukabaini kwamba mfumo wa pale ni mbovu,ikiwemo wa kukusanya Fedha,kwani wakawa wanakusanya wenyewe wakurugenzi fedha kwa wananchi na sio wahasibu wa Mamlaka hiyo,yaani wakawa wanafanya maksudi tu ili kujiwekea mianya ya kuiba  Fedha”
“ Yaani wakawa wanatumia fedha kwa manufaa yao na sio kupeleka kwenye miradi,hata pesa zenyewe walikuwa wanakusanya wakawa wanatembea nazo”amesema Waziri Wasira.
           Waziri Wasira ameongeza kuwa katika uchunguzi huo kamati hiyo pia ikabaini shilingi bilioni 2.9 zilizokusanywa  kwenye Mamlaka ya  Rubada, 715 milioni ndio zilizotumia kwenye miradi ya Wananchi  tu lakini Bilioni 2.5 zimeonekana kwamba zimeibiwa na yaani hazionekani zilipo.
          Waziri Wassira alibainisha kuwa mbali ya kuiba pesa hizo kamati ikabaini kwamba watendaji hao wametumia zaidi ya Milioni 314 kwenye matumizi ya kawaida ambapo anasema matumizi hayo ni makubwa zaidi ikiwemo pesa za zilizotengwa na maendelea ya miradi ya Mamlaka hilo zimepelekwa kwenye mipango ambayo anadai sio ya maendeleo.
      Vilevile Waziri Wassira amesema hata pesa ambazo wamewakata wafanyakazi kwa ajili ya kupelekwa kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii zimekuwa zikiliwa na watendaji hao tena kwa makusudi pasipo kupelekwa huko.
      Aidha,Waziri Wasira amesema baada ya kupata Ripoti ya Tume hiyo ameiagiza Bodi ya Mamlaka ya Rudaba kuwafukuza kama mara moja watendaji hao watatu na nafasi zako kujazwa mara moja huku, wakati taratibu na sheria za kuwafikisha mahakamani zikiwa zinafuata.

                Mamlaka  ya Rubada ambalo lipo wenye Bonde la mto Lufiji ambapo kazi yake ilikuwa ni wakuhudumia wananchi wanaotumia huduma za Bonde hilo.

pichani). Katikati ni Katibu Mkuu Bibi Sophia Kaduma (katikati), na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Dkt. Yamungu Kayandabila

No comments