Zinazobamba

HABARI KUBWA.ACT WAMCHIMBA MKWARA KIKWETE, KUHUSU KATIBA,SOMA HAPA KUJUA

Pichani ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama
 cha ACT-Tanzania
mama 
Anna Mughwira.
akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani
mda huu makao makuu ya chama hicho.
NA KAROLI VINSENT
CHAMA kipya cha siasa cha Alliance for Change and Transparence (ACT-Tanzania) ni kama kimeungana na Vyama vikuu vya upinzani nchi ambavyo vinaunda       UKAWA,baada ya kusema kitawahamasisha wananchi waipigie kura ya hapana katiba iliyopendekezwa na Bunge la maalum katiba.
Kwa madai katiba hiyo imejaa utata ambao unaligawa taifa kwa ujumla.
       Kauli hiyo imetolewa mda huu Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti Taifa wa Chama hicho, Mama Anna Mughwira wakati wa Mkutano na Vyombo vya Habari kwenye makao makuu ya ACT-Tanzania,ambapo amesema kikao cha kamati kuu ya chama hicho kilichokutana  mwishoni mwa wiki iliyopita walifikia maamuzi ya kuwataka wananchi kuipigia kura ya hapana katiba iliyopendekezwa.
        “Maamuzi ya kamati ya kuu ya chama cha  ACT-Tanzania, kwa pamoja tumewataka watanzania kwa ujumla kuipigia kura ya hapana katiba iliyopendekezwa na Bunge maalum la Katiba kutokana na katiba hii kutokizi vigezo vyake kwa mtanzania , ikiwemo kutoweka usawa pamoja  kutokuwa tunu za taifa”amesema Mama Mughwira.
         Mama Mughwira ameongeza kuwa Chama hicho cha ACT-Tanzania kikifanikiwa kuingia madarakani kitahakikisha kinaufuta kabisa mchako mzima wa kutafuta katiba mpya kutokana na upatikanaje wake wa sasa kutokuwa na vigezo vya kupata katiba bora.
       Kauli ya Chama hicho kipya inaendena na kauli walioitoa muunganiko wa vyama vikuu vya upinzani ambavyo vinaunda UKAWA ambao wao kwa pamoja waliwataka wanachama wao kutoipiga kura yeyote inayohusu kuipitisha katiba iliyopendekezwa.
           Mbali na UKAWA pia nalo jukwaa la kikristo nchini likiwa tayari limetangaza kwa waamini wa dini hiyo kuipigia kura ya hapana katiba hiyo.
         Katika hatua nyingine chama cha ACT-Tanzania kimesema kinatarajiwa kuanza ziara nchi nzima ambapo ziara hiyo yenye lengo la kukijenga chama hicho nchi na              kusambaza sera zao anazodai ni za mfumo wa kijamaa.

         Aidha,Chama hicho kimezidi kukanusha vikali tuhuma zinazotolewa kwenye chama hicho ambazo zinasema kwamba chama hicho ni Chama cha Mapinduzi CCM B,kwa kusema watu wanaosema hivyo wanajenda mbaya na yenye kutakiwa kupingwa kwani chama  hicho kinasera yake ya mfumo wa ujamaa ambayo wanadai chama cha mapinduzi hakina sera hiyo.

No comments