Zinazobamba

BREAKING NEWS-MACHAFUKO AFRIKA YA KUSINI,WAZIRI MEMBE AWAGEUZIA KIBAO WATANZANIA WALIOKO HUKO,SOMA HAPA KUJUA


SERIKALI nchini  ni kama imewageuzia kibao watanzania wanaoisha Afrika ya Kusini baada ya kusema itawarudisha nchini watanzania ambao wamekumbwa  tu na machafuko yanayo endelea nchini humo.Anaandika KAROLI VINSENT,endelea nayo
      Vilevile Serikali imesema ni watanzania 21  tu ambao ndio wamekubali kurudi nchini kati ya watanzania 23 waliokimbia machafuko yanayowakumba  wageni nchini Afrika ya kusini na kuhifadhiwa kwenye kiwanja kimoja cha mpira kilichopo nchini humu.
      Hayo yabainishwa Mdaa huu Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe Wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari ambapo amesema Serikali itawarudisha watanzania ambao wamepata matatizo ya kuvamiwa  ambao teyari serikali imeshawatambua,
     Na kusema kamwe Serikali haitamrudisha Mtanzania yeyote  ambaye atatumia machafuko hayo yanayoendelea nchi umo kama njia ya kurudi Tanzania, ambapo amedai kuwa wapo Watanzania wengi wakihangaika na maisha wakitaka kurudi nyumbani na kudai kuwa serikali haitoweza kuwarudisha wote kwani wako wengi sana wanaishi huko.
       Amebanisha kuwa jambo ambalo serikali inasubili kwa sasa ni kupata ruhusa kutoka kwa Ubarozi wa Tanzania alioko Afrika ya kusini ili kuwarejesha watanzania hao  waliokubali kurudi nchini,
   Aidha,Katika hatua nyingine Waziri Membe amekanusha Vikali taarifa zilizokuwa zimeripotiwa kwenye Mitandao ya Kijamii pamoja na baadhi ya magazeti wakidai kuwa watanzania watatu wamefariki kutoka na machafuko hayo
        Ambapo Waziri Membe amesema taarifa hizo ni  za uongo kwani Watanzania hao watatu wamekufa kutokana na magonjwa mbali mbali na sio sababu ya machafuko hayo
 Membe amewataja watanzania hao ni  Athumani China ambaye anasema mtanzania huyo amekufa kutokana na kupigwa na wananchi wa nchi hiyo baada ya kumpora mwenyeji wa huko.
      Mwingine ni Ally Mohamed ambapo pia amesema huyo naye amefariki kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa Kifua kikuu,pamoja na mtanzania mwingine aliyekufa gerezani alipofungwa ambapo alikufa kutokana na kuchomwa visu.
Vilevile Waziri Membe akawataka watanzania waishio nje ya nchi kupenda tabia ya kuwa pamoja ili matatizo kama hayo yaliyotokea Afrika ya kusini ili iwe Raisi kwa Serikali nchi kutoa msaada.


No comments