Zinazobamba

HUAWEI YAIPIGA JEKI MICHUANO YA GOFU YA KUMUENZI BETTY MALLABA,SOMA HAPA KUJUA

Mshindi wa Kwanza katika Mchezo huo, Hasnain Rahim (kushoto) akikabidhiwa Kombe na Mkurugenzi wa Mauzo wa Huawei, Samson Majwala.

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Huawei Mwishoni mwa wiki iliyopita imefanikiwa kuyadhamini mashinano ya kumuenzi aliyekuwa Rais wa Chama cha Wanawake cha Mchezo wa Golf Tanzania, Betty Malaba aliyefariki Aprili Mosi, 2010.anaandika Mwandishi wetu endelea nayo
         Katika kumuenzi mwanamichezo huyo, nahodha wa timu ya wanawake ya mchezo wa Golf, Hawa Wanyanche alisema kuwa wameamua kufanya mashindano hayo ili kumuenzi marehemu Betty aliyeweza kuwaunganisha na timu ya Tanzania kushiriki mchezo wa East and Central Afrika yaliyofanyika Uganda mwaka 2009 na Tanzania kuibuka washindi chini ya uongozi wake.



       Aidha ,Naye mwanachama wa mchezo huo, Victor Kimesera alisema kuwa licha ya marehemu Betty kuwa mwanamke, lakini aliweza kushinda vikwazo vyote vya wanawake katika kujitokeza kuchukua uongozi na pia uongozi alioweza kuchukua ni wa mchezo wa Golf ambao siyo wa wengi hapa Tanzania.

           Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Huawei Tanzania, Samson Majwala alisema kuwa kutokana na kutambua na kuthamini umuhimu wa mwanamke katika uongozi, hivyo wameamua katika kumbukumbu ya kumuenzi Marehemu Betty Malaba, kuyadhamini mashindano hayo na kutoa zawadi aina ya Huawei Ascend Mate 7.

          Aliongeza kuwa washindi ambao wameshinda katika mashindano hayo, wameweza kupata zawadi ya simu, Huawei Ascend Mate7 mbili, Talk Band pamoja na Router ya Internet ya 4G LTE yenye uwezo wa kutumia mtandao wa Smile Communication na kuahidi kuendelea kutoa zawadi kwa vikundi vingine.

       Walioibuka washindi katika mashindano yaliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana, jijinin Dar na kuijinyakulia zawadi mbalimbali ni Hasnain Rahim, Vikas Varma, Aliasger Mustafa, Ronald Phili na Fatuma Makame.

1.Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Huawei wakishikilia simu za kampuni hiyo.

2.Bango lenye nembo ya Simu ya Huawei.

3.Sehemu ya baadhi ya wageni waalikwa.
4.Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Huawei, Samson Majwala akizungumza jambo katika hafla hiyo.

5.Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Smile, Edgar Mapande (kushoto) na Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Huawei, Samson Majwala pamoja na Victor Kimesera mdau wa mchezo wa Golf.

6.Majwala akitoa zawadi kwa mshindi wa mchezo wa Golf.
7.Majwala akizungumza jambo katika utoaji wa zawadi hizo.
8.Majwala akionyesha zawadi ya simu ya Huawei Ascend Mate 7.
9.Mshindi wa mchezo huo (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Huawei, Samson Majwala.

10.Wahudumu wa Kampuni ya Simu ya Huawei wakishudia utoaji wa zawadi hizo.

1



No comments