Zinazobamba

MSANII WEMA SEPETU NA MILLARD AYO WAPAGAWA NA GARI LA MITSUBISHI ASX,SOMA HAPA KUJUA

Pichani ni gari jipya la mitsubishi ASX likizinduliwa rasmi wiki iliyopita 
Msanii maarufu nchini Wema sepetu akipanda Gari hilo jipya na la kisasa kabisa
Pichani ni Meneja mauzo wa Diamond \
Motors,Reena Ganatra
Akizungumza na waandishi wa Habari

MTANGAZAJI wa Clauds FM.Miladi Ayo na Mwigazaji maarufu nchini anayesifika kwa mbwembe mbalimbali,Wema Sepetu wamesifia gari jipya la Mitsubishi ASX la mwaka 2015,linalouzwa na kusambazwa na Kampuni ya Diamond Motors (Hansa Group)Anaandika KAROLI VINSENT,Endelea nayo.ubishi ASX kabla ya uzinduzi.
            Katika uzinduzi wa Kutambulisha gari hilo,uliofanyika mwishoni mwa wiki  jijini Dar es Salaam,pamoja na mambo mengine Kampuni ya Diamond Motors wauzaji pekee wa magari kutoka mitsubishi waliwaalika Milard Ayo na Wema Sepetu kujaribu gari hilo toleo jipya mitsubishi.
         Mastaa hao walivutiwa na mwonekano wa Mitsubishi ASX lenye vioo vya kisasa juu vyenye mwanga unaowezesha dereva kufurahia mwonekano wa upande zote.
        Meneja mauzo wa Diamond Motors,Reena Ganatra alisema Gari hilo lenye luninga ndogo inayocheza DVD,Ipods,Bluetooth na sauti kutoka vyanzo mbalimbali ni maalum kwa  vijana wa kisasa na Familia kwani Mitsubishi ASX.
        limetengenezwa na teknolojia ya MIVEC yenye kulifanya liwe na nguvu ya 150 ps katika 6,000 rpm na nguvu ya kuzunguka kwa mwendokasi mkubwa na kwamba limetengenezwa maalum kutumia mafuta madogo.
        Meneja huyo ameongeza kuwa injini ya gari ambayo ni 2.0 liter imeunganishwa INVECS-111CVT inayosaidia mwendelezo wake katika kubadili mwendo pamoja na uimara wa usukani unaosaidia mikono ya dereva kuwa salama hata unapokuwa Katika mwendo mkali.
        Aidha,Bwana Ganatra alisema kwa sasa gari hilo litauza kwa dola za kimarekani elfu 28 tu,na litakuwepo kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

     Vilevile Ganatra akawataka wananchi kuchangamkia fursa ya kununua magari hilo kwani ni kimbilio kwa watu wenye kipato cha chini.




 

No comments