Zinazobamba

HABARI ILIYOTIKISA JIJI-NAHODHA AJITOSA URAIS 2015 CCM,ASEMA ATAPAMBANA KUFA NA KUPONA SOMA HAPA


NA KAROLI VINSENT
HUKU  zikiwa zimebaki wiki chache Kabla ya chama cha Mapinduzi CCM akijapuliza Kipenga ili kuashiria kuanza kwa kampeni za makada wake kuwania nafasi ya Urais ili kumrithi Rais anayemaliza mda wake Jakaya Kikwete,sasa Kada mwingine wa chama hicho Shamsi Vuai Nahodha amejitokeza na kuitaka nafasi ya hiyo ya Juu ya nchi kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
     Kuibuka huko Waziri  huyo wazamani wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,kumekuja wiki moja tangu Rais Jakaya kikwete kusema kwenye Sherehe za miaka  38 ya CCM yalifonyika mkoani Songea na kuwataka wananchi washawishi makada wengine wenye sifa wajitokeze kwenye nafasi ya Urais na kuongeza mgombea atakayerithi mikoba yake bado ajajitokeza.
      Nahodha ambaye aliwaikuwa kiongozi wa juu huko Zanzibar ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na FULLHABARI.BLOGS ambapo pamoja na mambo mengine alisema kwa sasa yeye anaitaka nafasi hiyo ya urais kwenye uchaguzi mwaka 2015 ndani ya chama hicho, kwa kujinadi naye anafanya kimya kimya,kwani amebaini anazo sifa zote.
      “kiukweli mimi ninazo sifa zote za  kuwa kuiongoza Tanzania katika miaka 10 ijayo, kwani ninasifa zote,nimekuwa muadilifu sana, tena ni kiongozi mwenye uwezo,nakuhakishia rasmi najitosa na mimi kwenye kupambana na wengine waliojitokeza”alisema Nahoza.
              Nahoza aliongeza kuwa uzoefu aliokuwa nao katika kuongoza nafasi nyeti ya wizara ya ulinzi na kusema unampa imani ya kuweza kuwatumikia wananchi.
“Mimi ni kuongozi mzoefu wa masuala ya ulinzi,nimeongoza wizara ya ulinzi bila matatizo yeyote na nakuhakikishia hata ukienda kwa wanajeshi wote wanatakwambia mimi ni mtu gani,”aliongeza Nahodha.
         Alipoulizwa amejiapanga vipi kupambana makada wenzake wa Chama hicho wanaotumi pesa na wamejiapiza kufa na kupona ili kushika nafasi hiyo anayoitaka ili wapate nafasi hiyo alisema “Kiukweli nakuhahakishia kutangaza nafasi hii naingia kwenye mapambano makubwa naimani nitafanikiwa na historia yangu inaniruhusu kushindana nao”
       Kuibuka huko kwa Nahonda kunaongeza idadi ya makada ndani ya Chama hicho wanaowania Urais baada yaWaziri  wa Maliasili Lazoro Nyalandu, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyesema ametangaza nia kimyakimya.
        Mbali na hao waliotangaza nia, wapo wanasiasa ambao wamekuwa wakitajwa kuwa miongoni mwa wanaotaka nafasi hiyo ambao ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya.
          Wapo pia Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk Mohamed Gharib Bilal na Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha - Rose Migiro

Hakuna maoni