Zinazobamba

RAIS KIKWETE--NI VIGUMU KUIMALIZA FORENI YA JIJINI LA DAR,ASEMA NI ISHARA YA MAENDELEO SOMA HAPA ZAIDI

PICHANI RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWAHUTUBIA WAKAZI WA TEGETE JIJINI DAR ES SALAAM,WAKATI WA UZINDUZI WA BARABARA KATI YA MWENGE HADI TEGETA
Na karoli Vinsent
RAIS Jakaya Kikwete amesema Tatitizo la Msongamano wa Magari katika Jiji la Dar es Salaam ni vigumu kumalizika haraka,bali serikali yake inajipanga kuhakikisha inalipunguza tatizo hilo,
Kwa kuanzisha usafili wenye haraka kama mradi wa mabasi yaendeyo kwa kasi (DART) ,na usafili wa reli yaani treni.
         Rais Kikwete amesema hayo leo Jijini Dar Es Salaam wakati wa Uzinduzi wa barabara ya bagamoyo inayoanzia Mwenge hadi Tegeta,ambapo Rais Kikwete amesema ni vigumu sana tatizo la msongamano wa Mgari kumalizika kabisa kutokana na ongezeko kubwa la watu wanaomiliki Magari,

PICHANI NI RAIS KIKWETE KULIA AKIWA NA BAROZI WA JAPANI NCHINI MASAKI OKADA AKIKATA UTEPE IKIASHILIA UZINDUZI RASMI WA BARAARA KATI YA MWENGE HADI KAWE,PICHA NA IKULU
         Na kusema tatizo la msongamano wa magari katika nchi nyingi Duniani hususani maeneo ya katikati ya Jiji wameshindwa kuondoa tatizo hilo zaidi ya kuweka usafili utakao wafanya wananchi wasitumia magari binafsi.

“Kukweli acha niseme ukweli tatizo la msongamano wa magari katika jiji hili ni vigumu kuisha,hebu jiulizeni wote tatizo hili lilikuwepo miaka ya nyuma jibu ni hapana kutokana na kipindi kile watu wenye magari walikuwa wachache tena wakuwahesabu lakini sasa kila mtu anagari,tena wote wanataka kuja mjini”
HUU NDIO BARAARA ILIVYO SASA 
        “Na wakifika katika makutano ya magari lazima walete foreni tu ndio maana serikali imeona njia raisi ni kuanzisha usafili wa haraka utakokufanya uacha gari lako nyumbani na utumie usafili wa haraka na tayari tumeanza kwa kuanzisha usafili wa Mabasi yaendayo kwa kasi na tuko mbioni sasa kuanzisha usafili wa reli yaani treni”alisema Kikwete
       Aidha Rais Kikwete aliitumia nafasi hiyo kuipongeza serikali ya Japani kwa msaada mkubwa wa kifedha na kitaalamu katika ujenzi wa Barabara hiyo,ambapo amesema barabara hiyo itawasaidia wananchi wa jiji la Dar Es Salaam.
          Awali akizungumia mradi huo barabara Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi muhandisi Mussa Iyombe  amesema Barabara hiyo yenye kilomita 12.9 kutoka mwenge hadi kawe Jijini hapa ujenzi wake ulianza mwezi februari mwaka 2012 na kazi ya ujenzi rasmi ujenzi wke ulianza mwezi desema mwaka huo ambapo hadi kukamilika kwake umeghalimu Bilioni 99.9 za kitanzania ambazo kati ya hizo asilimia 95 ni za msaada kutoka serikali ya Japani.

     Kwa upande wake Barozi wa japani Nchini Masaki Okanda alisema Serikali ya Japani haitoacha kuisadia serikali ya Tanzania katika mambo mbalimbali ikiwemo barabara na kuwataka watanzania kuitunza Miundominu ya Barabara.

Hakuna maoni