Zinazobamba

INASIKITISHA-HIVI NDIVYO SAMWEL SITTA ALIVYOCHAKACHUA KURA ZA WAJUMBE UPANDE WA ZANZIBAR,ILI KUIPITISHA KATIBA YA CCM.SOMA HAPA KUJUA ZAIDI

Samuel Sitta
Na karoli Vinsent
      MCHEZO mchafu uliofanywa na Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta wakati wa kupata seluthi mbili kwa upande wa Zanzibar ili kupitisha Rasimu ya Katiba ya Chama cha Mpinduzi Imefichuka Mtandao huu umebaini.
Habari za kuaminika ambazo Mtandao huu umizipata kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa CCM, zinasema kuwa akidi inayotakiwa kutoka Zanzibar kupitisha Katiba inayopendekezwa, ilikwama lakini ilibidi kura zichakachuliwe kukidhi matakwa ya kisheria.
          Mtandao hu umebaini Mchanganuo wa kura halisi uko hivi; Wabunge wote wa Bunge Maalum la Katiba, wako 629 kati yao 419 wanatoka Tanganyika na 210 wanatoka Zanzibar.

              Wajumbe wanaotoka Zanzibar wako 210 na theluthi mbili yao ni 140. Wajumbe wa UKAWA kutoka Zanzibar waliotoka bungeni, wako 67 na wajumbe kutoka Zanzibar waliopiga kura ya hapana wako wanane.
         Na ili kuinyima Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa isipite, kura 71 ambayo ni theluthi mbili (2/3) ya Zanzibar ilitosha kabisa kukwamisha mchakato huo.
          Hivyo wajumbe 67 wa UKAWA wakijumuishwa na wajumbe saba waliosema ‘Hapana’, wanapatikana 75 hivyo waliopitisha katiba inayopendekezwa ni chini ya 135.
          Mtandao huu pia umebaini, Idadi ya wajumbe wa UKAWA, ukiongeza kura mbili, moja ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, Abdallah Abas na Othamn Masoud, kisha kuchanganya za wale wajumbe waliopiga kura ya Hapana, jibu liko wazi akidi haikutimia.
          Vilevile UKAWA walihitaji kura 71 tu kuzuia Katiba ya Mpya, wajumbe 67 ukiongeza na wajumbe wawili, Othamn Masoud na Abas, idadi ya wajumbe inafikia 69 na ukiongeza kura zilizosema ‘Hapana’, akidi ya Zanzibar haitatosha.
            Hesabu hizo ni bila kuzingatia matokeo ya kura zilizopigwa kwa siri na waliopiga kura wakiwa nje ya Bunge Maalum.
            Mtandao huu ukadokezwa Hata kama kura zote zingekuwa zimeikubali katiba inayopendekezwa zisingeweza kubadilisha uhalisi na ukweli wa kitakwimu za kukosekana kwa akidi.
Kwa uchunguzi wa uliofanywa na Vyanzo mbalimbali unasema  theluthi mbili ya kura za wajumbe wote wa Bunge la Katiba wanaotoka Zanzibar haikuwapo na kilichofanyika ni uchakachuaji ili kupisha katiba iliyojaa mapendekezo ya ccm.


Hakuna maoni