Zinazobamba

HAMMADI TAO NANI AMEKUROGA, POSHO ZA LUKUVI ZITAKUUA


 https://zanzibariyetu.files.wordpress.com/2014/04/lukuvi.jpg?w=584&h=438

Wanaharakati wa kislam hapa nchini wamehoji hatua ya taasisi inayojishugulisha na kujenga undugu kati ya waislam na wakiristo hapa nchini ya kumuomba Mh. Rahis wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuifuta jumuiya ya uamsho na mihadhara wakidai kuwa hatua hiyo inamkono wa mtu na sio bure
Wakizungumza na mwandishi mwandamizi wa mtandao huu hivi karibuni, Shehe Basareh amesema, kikundi hicho kinatumiwa na wale wote ambao hawautakii mema uislam.
Amesema kuibuka kwa kikundi hicho na kuanza kumuomba rais kufuta taasisi ambao ipo kihalali na ambayo haijakutwa na makosa yoyote ya kuhusika na tuhuma zinazotajwa na wanaotaka kuua uwepo wa taasisi ni wazi kuwa lengo lao la kutaka kuua viongozi wa kikundi hciho kinazidi kujidhilisha,

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjL0k1EBYVpsjipq263wSZbvLyYnqQ8B3Ez-vV_kwH5f13Zwm9nqjJGzKXIvipZSAs-dsLSPxyFBGDUgAin14xCKa0kqlw4yDarda_hsD4cLfvYoJWUdknljmZ7cWdwRV5HAr6OB_T0zfE/s1600/uamsho.JPG
Amesema, tokea kumezuka kwa tuhuma lukuki dhidi ya Uamsho hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza hadharani na kuleta ushahidi wa kusadikika wa tuhuma husika na badala yake kila mmoja amekuja na Dhana ambayo kiukweli inaongeza hasira kwa viongozi na waislam kwa ujumla,
Hata huyo anajiita Hammadi Tao, kabla ya kupokea milungura kutoka kwa huyo mfadhili wake, kwanza angejiuliza kabla ya kuchukua maamuzi hayo, je kunaushahidiwowote wa kuaminika kuwa JUMUIK imehusika na tuma za kigaidi huko Zanziabar, Aliosema Basereh

Huko ni kutumika kwa baadhi ya taasisi za kiislamu kuwachafua waislam wenzao, madhalim wanajua wazi wakiwatumia viongozi wa kidini basi waislam wataamini hoja zao na kuwafuata, lakini ukweli ni kwamba hao wajenga udugu wametumika na hakuna wa kubisha katika ukweli huo,
Tunawaomba wale vizuri hizo pesa zao za kuhongwa, waache kuchafua watu kwani kufanya hivyo ni dhambi kubwa kwa mungu na watachomwa.. Aliongeza.
Hivi karibuni Kikundi cha kujenga udugu kati ya waislam na wakiristo walimpigia magoti rais na kumuomba kukifuata  kikundi cha mihadhara ya kiislam Tanzania maarufu kama UAMSHO kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kikundi hatari na hakiitakii mema nchi ya Tanzania
 Ombi hilo lilitolewa na  HAMAD TAO ambaye ni mwenyekiti wa taasisi inayojihusisha na kujenga undugu kati ya dini ya CHRISTIAN AND MUSLIM BROTHER HOOD SOCIETY ambapo katika mkutano na wanahabari  taasisi hiyo imesema kuwa kikundi cha uamsho hawana lengo nzuri na nchi ya Tanzania kuutokana na matamko yake ambayo imekuwa ikiyatoa ya vitisho dhidi ya watu mbalimbali pamoja na dini nyingine ambapo amesema kikundi hicho kinasababisha uhasama baina ya dini na dini.
Katika mkutano huo na wanahabari,  HAMAD TAO ambaye ni mwenyekiti wa taasisi hiyo amesema kuwa kikindi cha uamsho hakina tofauti na vikundi vingine vya kidaidi duniani huku akienda mbali na na kukifananisha na vikundi kama ALCAIDA,BOCO HARAM NA ALSHABABU.
“sisi tumekuja hapa kwa upendo na kuipenda nchi yetu tunaiomba serikali ya Tanzania isiwafungie macho hawa watu wanaounda kikundi hiki kwani ni hatari kwa amani tuliyonayo”alikaririwa Bw. Tao
Aidha taasisi hiyo imesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kikundi hicho cha UAMSHO matukio ya kigaidi Zanzibar kama kumwagiana tindikali,makanisa kuchomwa moto na ugaidi mwingine umekuwa ukiongezeka kwa kasi huku wakikwepa kuwahusisha uamsho moja kwa moja kuhusika na uhalifu huo.

Hakuna maoni