Zinazobamba

UAMSHO HAWATA PONA, MAUAJI YANUKIA

Mjumbe wa uamsho akifafanua jambo, katika moja ya vikao vyake na waandishi wa habari jijini Daresaalam

Unaweza kusema sasa jumuiya ya uasho na mihadhara ya Zanziaba r haita pona kufuatia mbegu mbaya inayopandikizwa kwa wananchi na viongzo wa ngazi za juu hapa nchini kuichukia jumuiya kutokana jumuiya hiyo kuhusika na matendo ya kigaidi katika shuguli zao za kila leo
Utafiti uliofanywa na mwandishi wa habari hzi umebaini, utata mkubwa dhidi ya tuhuma zinazoelekezwa kwa jumuiya hiyo, huku wale wote wanaowanyooshea kidole jumuiya hiyo wakiwa hawana ushahidi wa kusadikika wa kuwachukulia hatua taasisi hiyo,
Katika kuonyesha kuwa viongzi wa ngazi za juu wamepania katika mipango ya kuibobomoa tasisi hiyo kwa njia yoyote hata kwa mtutu, kumeonekana sasa kuna watu wameanza kujitokeza hadharani wakiwahukumu jumuiya hiyo kuhusika na vitendo vya kigaidi huku wakiwa hawana ushadi wa kutosha  dhidi ya watuhumiwa husika
Miongoni mwa viongzoi wakubwa ambao wamejitokeza hadharani na kuwasema vibaya jumuiya hiyo ya kiislamu hapa nchini ni Mh. William Lukuvi wakati akimuwakilisha waziri mkuu katika moja ya kanisa huko mjini Dododma,
Katika hotuba ambayo, Waziri huyo wa ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa Bunge, amesikika akiwatuhumu jumuiya hiyo, na kuirudia tena kauli yake katika bunge maalum la katiba pale alipomuunga mkono Mh. Mrema  kwa kusema uasho walihusika na vitendo vya mauaji ya padre, uchomaji wa makanisa pamoja na uharibifu wa miundo mbinu huku wakijua wazi wanachokisema hawana ushahidi navyo.

Kwa hali ilivyo, na wiwa kusema ili mtu ukitaka umuondoe katika ramani, ni lazima umfanye asiwe wa thamani katika jamii husika ili hata kama akiondoka aonekane, na hilo ndilo wanalolifanya viongzoi wakuu wan chi hii dhidi ya jumuiya ya waislamu ya mjini Zanziabar,
Hivi karibuni, jumuiya hiyo ilikuja juu na kumtaka wziri huyo kupeleka ushahidi wa tuhuma alizozitoa dhidi yao na kwamba akishindwa kufanya hivyo basi sheria ichukue mkondo wake, ikiwemo yeye mwenyewe kujiudhuru ama rais aliyemteua kuichukua dhamana hiyo aliyompa ili kunusuruu vita ya kidini hapa nchini,
Imeitwa ni vita ya kidini kufuatia ukweli kuwa alihusika kutoa tuhuma alikuwa kanisani na wanaowatuhumu pia ni wa upande wa pili, sasa kwa vyovyote vile upande huo wa pili hautakuwa tayari kuona wenzao wakinyanyasika.
Hebu angalia Mfululi wa tuhuma za uamsho
Mwaka 2004
Jumuiya  ya uasho na mihadhara ya kiislamu JUMUIK ilituhumiwa kuhusika na vulugu zilitokea huko Zanzibar  ikiwemo milipuko ya mabobu,kuchomwa kwa makanisa,kuchomwa kwa gari ya polisi, na kuharibiwa kwa miundo, Kufuatia tukio hilo Tume mbili ziliundwa kuchunguza ukweli wa kadhia hiyo . Tume hizo ni ile ya maziwa makuu na Tume ya kamati maalum ya jeshi la polisi likiongozwa wakati huo na aliyekuwa mpelezi mkuu wa makosa ya jinai Bw. Robert Manumba,
Tume hizo mbili mpaka sasa yapata kipindi cha miaka kumi lakini bado tume hizo zimeshindwa kutoa taalifa yeyote ya utafiti wao kuhusiana na kadhia ya kipindi kile, japokuwa walitangaza hadharani tume ingeweza kumaliza majukumu yake  na kutoa taarifa ndani ya  kipindi cha mwezi mmoja,
Mwaka 2012
Matukio kama yaleyale ya mwaka 2004 yalijitokeza tena, mnamo mei 26-29 mwaka 2012 , wimbo ukawa uleule wa kuihusisha jumuiya hiyo ya kiislam kushiriki katika vitendo vya kiuhalifu huku uthibisho wa ukweli halisi wa taarifa ukishindwa kuonyeshwa mbele ya jamii, . kufuatia  kuandamwaandamwa na kupewa majina mabaya ya kuhusika na vitendo vya kihalifu mjini Zanzibar, Juiya hiyo ilikaa chini na kutafakari wanafanya nini ili kutoa ukweli halisi kwa jamii, Ndipo walipoamua kumuandikia Barua Rais, wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shei mnamo tarehe 03june 2012 ikimuomba rais huyo kuunda tume ili ukweli ujulikane ,

Lakini kwa bahati mbaya mpaka leo hii hakuna tume yeyote iliyoundwa ili kubaini ukweli wa majina mabaya ambayo Jumuiya hiyo inapewa na watu wachache ambao hawaitakii mema jumuiya, kutokana na maslahi yao yenyewe yawe ya kisiasa ama ya kiuchumi,
KAULI YA LUKUVI , MREMA,
Katika hatua ya kushangaza, kiongozi mkuu kabisa wa serikali ambaye ni waziri wa Nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge, hivi karibuni ameibuka na hoja zilezile za kuzihusisha jumuiya hiyo ya kiislamu kuhusika na matendo ya kihalifu akiwa kanisa moja huko Mjini Dodoma,

Lukuvi alikaririwa akimuunga mkono Mh. Mrema kuwatuhumu Uamsho kuhusika na vitendo vya kiharifu ikiwepo kuuliwa kwa padre, kuchomwamoto kwa makanisa na uharibifu wa mali za umma na miundo mbinu kitu ambacho waliwahi kutuhumiwa wakati huo na majibu yake viongozi kuyakaria
Dhana ya uamsho kujihusisha  na chama cha CUF.

Kunatuhuma zingine za jumuiya hiyo kuhusishwa na chama cha kisiasa wakidai kuwa sera za chama cha CUF zinaendana na sera za Jumuiya hiyo ya uamsho na mihadhara kauli ambayo katibu mkuu wa jumuiya hiyo Abdalah Said Ali ameikanusha vikali tena mbele ya hadhala, na sio CUF tu bali jumuiya hiyo haina uhusiano wowote na chama cha siasa ndani ya Zanziba wala huku bara.

Mjumbe wa jumuiya hiyo ya uamsho ambaye pia ni mkurugenzi wa elimu na habari, alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuna mipango inasukwa ya mauaji dhidi ya kikundi hicho, na kwamba siri hiyo imegundulika. 

Mjumbe huyo alisema waliogundua uwepo wa mipango ya mauaji ni miongoni mwa polisi ambao wengine tayari wameshacha kazi kutokana na mipango hiyo kuwahudhunishwa

Tumeshaambiwa kuwa kuna mipango ya mauaji, na ndio maana wameanza kwa kutupandikizia uadui kwa raia ili tujulikane sisi ni magaidi, tumejua janja yao tunasema na kuwaomba serikali iachane na mipango ya kuua raia wake

Sina hakika kama Nchi yetu itaingia vitani lakini , kama hatua za haraka hazitachukuliwa ninaona harufu mbaya dhidi ya uamsho, na hapo ndipo ninapopaogopa mimi, alisema mmoja wa wadau waliohojia dhidi ya tuhuma wanazopewa jumuiya ya Uamsho.

Hakuna maoni