Zinazobamba

RUBADA WAPATA BODI MPYA,CHIZA AWATAKA WAINASUE MAMLAKA HIYO



Mkurugenzi wa mamlaka ya mto rufiji, Bw. Aloyce Masanja akijibu moja ya hoja zilizoelekezwa kwake mapema hii leo, Masanja amesema kuna haja ya kutungwa kwa sheria ili kuinasua mamlaka sifife. Aliyekaa kushoto kwake ni Mwenyekiti wa bodi hiyo, Prof. Msambichaka Luciani.


Naibu waziri wa chakula na kilimo, Mh. Godfrey Zambi akifafanua jambo katika uzinduzi wa budi hiyo, zambi amewataka wafanyakazi wa  wa mamlaka hiyo kuwapa ushirikiano wa kutosha bodi hiyo ili iweze kuondoa changamoto za mamlaka.





Na mwandishi wetu,
Waziri wa Chakula na Kilimo, Mh. Cristopha Chiza ameitaka bodi mpya iliyoingia madarakani  katika mamlaka ya maendeleo yam to rufiji (RUBADA)kuhakikisha wanafanya jihida za kuikwamua mamlaka hiyo ambayo kwa sasa imeonekana kama haina faida miongoni mwa macho ya watanzania ambao wanaona majuku mengi ambayo yanayofanywa na mamlaka hiyo tayari tayari zinafanyawa na taasisi zingine,

Akizungumza na bodi hiyo mpya alioizindua mapema hii leo, Dk Chiza amesema kazi kubwa ambayo bodi hiyo inayo kwa sasa ni kubadilisha taswira ya mamlaka hiyo ambayo  kwa sasa siyo nzuri kutokana kuonekana kama haina umuhimu kufuatia kazi zake kutojulika na hata mipaka yake ya uwajibikaji kutokuwa wazi,

Chiza amesema, lazima wahakikishe kuwa taswira hiyo ya kudhaulika hadi kufikia hatua ya baadhi ya watu kupendekeza kufutwa kwa mamlaka hiyo inabadilika na kuwa mamlaka yenye meno na kusimamia vizuri majuku yake katika maeneo  ambayo yataainishawa ,

Najua mnaingia katika mamlaka hii mkiwa  na kazi nzito ya kubadilisha taswira ya mamlaka na kuifanya mamlaka itakayosaidia serikali kwa kuhakikisha mnatunga muswada wa sheria utakaohakikisha mnapewa majukum yenu ya kuyasimamia ipasavyo, ili muweze kuonyesha kazi mnayofanya kwangu na kwa rais kwa ujumla. Aliongeza Dk Chiza.

Aidha Chiza ameitaka bodi hiyo kufanya kazi kwa karibu na utawala uliopo ili kufikia malengo ya kuiboresha taasisi hiyo kwani kwa kufanya kazi pamoja kutaleta tija katika utekelezaji wa majukum ya kila leo ya Mamlaka,

Naye Mwenyekiti wa bodi hiyo ya Rubada  Prof. Msambichaka Lucian, amesema kuwa wamechukua changamoto ambayo imetolewa na Mh. Cheza na kwamba kwa kuanzaia wameamua kuanza kujipa malengo ya kupeleka taarifa ya utekelezaji wa majukum yao ya kila kwa  waziri kila baada ya miezi mitatu ili kumuonyesha waziri ni namna gani wamejipanga kuifufua taasisi hiyo ambayo ilikuwa inaelekea kufa,

Kwanza tunashukuru kwa muheshimiwa waziri kutambua changamoto iliyo mbele yetu, lakini tunamuhakikishia muheshimiwa huyo uwajibikaji wa kiwango cha juu, ili asione kama kuteua bodi hii amefanya makosa ya hali ya juu,

Tunafahamu kuwa changamoto ni kubwa ya kuondoa matatizo katika sekta hii ya kilimo lakini tumejipanga kuondoa vikwazo vyote, kwa kuanzia tutaandaa muswada ambao kama waheshimiwa wabunge wataupitisha basi tunadhani hii tabia ya muingiliano wa majukum kati ya wizara moja na nyingine itaisha,

Utaona hapa Lubada, tumefanya tafiti nyingi nzuri lakini hakuna anayetumia tafiti hizi na watu wanaamua kuanza kuandaa tafiti zingine wakati hapa tafiti zipo tena za kitu hichohicho wanachofanyia tafiti, tunadhani kutokuwa na muundo mzuri wa uwajibikaji ni tatizo na ndio maana sisi tumeletwa kuondoa sintofahamu hiyo katika mamlaka hii, Aliongeza Prof. Lucian

Naye mkurugenzi wa mamlaka hiyo ya RUBADA Bw. Aloyce L. Masanja, ametaja changamoto nyingi zinazoikabili taasisi hiyo kwa sasa, moja wapo ikiwa ni muingiliano wa majukumu kati ya kituo cha uwekezji na mamlaka yake hatua ambayo inaonyesha wazi kuwa kuna haja ya kufanya marekebisho makubwa ya sheria iliyoipa mamlaka  taasisi hiyyo kuanzishwa kwake,

Amesema muarobani wa kuinasua RUBADA kwa sasa ni kuundwa kwa sheria mpya ya mamlaka itakayoweza kuainisha kazi zao ili kazi zao zisiweze kuingiliana na mamlaka zingine

mwishoooo


Hakuna maoni