Zinazobamba

WADAU WASEMA JUKWAA LA KATIBA HALINA SIFA YA KUSULUHISHA MGOGORO BUNGE LA KATIBA, MGEJA NAYE ATIA NENO



Sifa pekee ya refarii, ni kuwa mtu ambaye hana mapenzi na moja ya pande ambazo wanapambana katika soka, Kama ikitokea refarii huyo anakuwa na upande ambao anaushabikia basi refaa huyo huambiwa amepoteza sifa ya kuwa refa na hivyo jitihada za kutafuta refa mwingine kuchezesha mpambano huo itachukuliwa,


Katika masuala ya soka hali hiyo ni ya kawaida sana, Tumeshuhudia baadhi ya klabu maarufu sana hapa nchini zikiingia katika mgogoro wa refarii, wengine wanasema huyo ni refa wa Yanga, Huku nao simba wakisema huyo ni refa wa simba, timu singine utasikia huyo refa kapewa mlungura basi imekuwa ni hivyo kila mmoja hana imani na refa ambaye amejimbambanua kuwa na upande ambao anaushabikia,


Hivi karibuni Jukwaa la katiba hapa nchini, lilijitokeza hadharani na kutangaza kuomba fulsa ya kuwa wasuluhishi wa migogoro itakayokuwa ikiibuka pale mjengoni, mjini Dododma,


Jukwaa walifikia hatua hiyo baada ya kuona kutokuelewana kati ya ukawa na wajumbe wengine katika bunge maalum la katiba, huku wakisema wazi kuwa kutokuelewana huko hakutoishia tu kwa ngazi ya ukawa na Tanzania kwanza, kwani huko mbele tunakoenda inaonekana wazi kuwa migogoro itakuwa mikubwa isivyo kawaida kutokana na ukweli kuwa maslahi ya watu yataanza kujadiliwa ,

Wakulima watatetea maslahi ya kundi lao, wafugaji watatetea maslahi ya kundi lao, huku wabunge wa kisiasa nao watatetea maslahi ya ukomo wao wa kuwa wabunge hapo ndipo mgogoro wenyewe utakapoanza na huku nje kanuni na sheria zote zikiwa kimya juu ya migogoro hiyo itakapotokea itapelekwa kwa nani,



Kufuatia hali hiyo jukwaa wameliona hilo na wamekuja na muarobaini wa kuomba tenda ya kuwa wasuluhishi wa migogoro yahapo mjengoni, wameanza kuwaleta kundini majaji maarufu ukanda wa Afriaka mashariki na kati na Dunia kwa ujumla, ambao kwa muda mrefu hawajaonyesha kuwa upande fulani ili kufanya kazi nao ya kutatua migogoro ya Mjengoni


Miongoni mwa majani ambao wamewaleta kundini ni pamoja na Jaji Banabasi Samata, ambaye kwa muda mrefu amekuwa kimya katika mchakato huu wa katiba na hajaonyesha wazi kwa jamii kuwa yeye yuko upande gani, hatua ambayo imeonyesha wazi kuwa yeye ni refarii mzuri katika suala migogoro,


WANANCHI WAHOJI UHALALI WA JUKWAA KUWA REFARII

Licha ya nia yao njema ya kuhakikisha migogoro katika bunge maalum la katiba yanapatiwa ufumbuzi, bado wananchi wamejitokez ana kusema waziwazi na mtandao huu kuwa jukwaa la katika halina sifa ya kuwa refarii wa mchakato kutokana na ukweli kuwa tayari wameonyesha upande ambao wanaushabikia


Wakizungumza na mwandishi maalum wa Mtandao huu hivyi karibuni, mmoja wa wanaharakati makini sana, ambaye hakutaka majina yake kutajwa katika mtandao huu amesema, tokea azaliwe na kuanza kuisikia itikadi ya jukwaa la katiba haijawi hata siku moja kuonyesha wazi kutaja hata mazuri yanayofanywa na serikali ya chama cha  CCM, hatua anayoitafsiri kuwa Jukata tayari wana mlengo katika kufanya kazi zao,


Amesema Chama cha mapinduzi hakiamini kama JUKATA wanaweza kuwa wasuluhishi wazuri wa migogoro itakayotokea kule bungeni, na badala yake watakuwa wanapendelea kina ukawa, na kukandamiza hojaza CCM hatakama zinamashiko kiasi gani,

Kufuatia ukweli huo ni wazi kuwa tayari haki ya wao kuwa marefa imepotea kama wao JUKATA walivyotangaza kuipoteza haki ya Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuwa mmoja wa wasuluhishi wa migogoro ,wakidai kuwa rais amepoteza sifa hiyo kwa kuingilia mchakato na kutangaza nia yake hadharani ya kutetea serikali mbili ya chama chake


Amesema hata kama kuna vitisho kiasi gani kuhusiana na kupotea kwa amani na kufanyika kwa machafuko hapa nchini kutokana na kutokuwepo kwa msuluhishi ni bora kuliko kuwa na msuluhishi ambaye tayari ameonyesha ushabiki wa wazi wa upande fulani,

Tunadhani kuna haja ya kuwepo wasuluhishi hata kama wanatoka nje, lakini hawa JUKATA wamepoteza sifa nahivyo hawastahili kubeba jukumu hilo zito ambalo kama watapewa watu kwa kutoangalia vigezo maalum tunaweza kuongeza tatizo kuliko kutatua tatizo kama JUKATA wanavyosema. Aliongeza



    MGEJA AFUNGUKA,

Kwa upande wake mwasiasa nguli wa CCM , Toaka mkoa wa Shinyanga, Bw. Khamis Mgeja amebuka na kusema kuwa hatua iliyotangazwa na Jukwaa la katiba ni ya kupongezwa na kwamba wanastahili kupewa jukumu hilo kama kweli wamedhamilia kuondoa migogoro katika mchakato wa uundaji wa Katiba mpya,

Amesema mchakato wa katiba mpya si wa mtu ama chama fulani bali ni mchakato wa wote na kwamba mchakato ukiharibika asijekuonyeshewa kidole mtu yeyeto kwani saa ya kufanya marekebisho ni sasa, kusbuli hali iwe tete hakutaleta tija  hata kidogo .

Katika hatua nyingine Mgeja ametoa wito kwa wafuasi wa ukawa na wale wajumbe wa ukwa kuachana na tabia ya kususa, kwani tabia hiyo haitajenga katiba na badala yake  basi wajipime ni namna gani wanaweza kujenga hoja na kuwashawishi wenzao ili waweze kukubaliana kwa hoja na sio kuwa na msimamo ambayo haitakuwa na tija kwa mustakabali wa katiba mpya.

Hakuna maoni