Zinazobamba

Mbeto :OMO asiwanie urais zbar kwa kutegemea hadithi za vijiweni

Mweyekiti  wa ACT  Wazalendo,  Othman Masoud Othman ,  kutotia nia ya kuwania urais Zanzibar kwa  kuziamini  hadithi za  kale  za vijiweni na Mitaani  zinazodai ati   CCM hakijawahi kushinda.

Pia   CCM  kimekumbusha asidhani kwa  kulitumia jina la Hayati  Maalim  Seif  Sharif  Hamad , kutamzidishia  chochote ili akwepe kipigo cha kushindwa  vibaya. 

Hayo yameeelzwa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar, Khamis Mbeto  Khamis,  aliyemtaka Othman,  ajiandae kukumbwa na kimbunga kuliko kilichowahi kummkuta mgombea mwenzake wa upinzani

Mbeto alimtaka  OMO aache kuziamini hadithi  zinazodai  CCM  hakijawahi kushinda wakati  ushindi wake ndio  unaounda  Serikali  toka mwaka 1995 hadi sasa huku  yeye (Othman)  akiwa sehemu  ya watumishi chini ya SMZ

Alisema ni upuuzi kwa  mtu mzima kama Othman kuamini CCM  hakitashinda  wakati   serikali ya CCM  ndiyo inayomlipa mshahara  ,imekuwa akimpatia nyumba anayoishi na familia  yake , magari ,ulinzi na huduma nyingine  muhimu . 

'Othman jiandae kushindwa kama alivyushindwa mgombea mwenzako  kuanzia mwaka 1995 hadi 2020. Kila  CCM iliposhinda na kuunda Serikali  wewe umekuwa  kati  ya watumishi  wake watiifu  SMZ waliopatiwa ajira " Alisema Mbeto 

Pia  Katibu  huyo Mwenezi  alisema madai ya kuwepo uvunjaji wa haki za binadamu na kutofanyika mageuzi ya kiuchumi ni maneno yasioingia akili  wakati Zanzibar ya leo ikiizidi kumeremeta kimaendeleo .

'Acha  kuwania urais wa Zanzibar  kwa kutegemea ubebwe na jina la marehemu. Midhali umetaka uwekwe utangani na kufindwa,  jiandae  kuchezwa unyago waliochezwa wenzako "Alieleza

Mbeto alisema Othman ameamua  kuchukua fomu  ya kuwania urais  katika wakati  ambao  smz chini  ya Rais  Dk Hussein Ali Mwinyi  imefanya mageuzi  makubwa ya kimifumo,kitaasisi  ,kisheria na kuziweka sawa hali za maisha ya wananchi .

" Mgombea wa CCM hakumbushi tawala za kikoloni zilivyodumaza maendeleo ya Zanzibar  .OMO  anapokumbusha mambo yaliojiri  mwaka 1995 nae  akiwa  sehemu ya smz ni kukichezea shere chama chake " Alisema 

Katibu huyo  Mwenezi  alisema kama kweli Othman  anaamini  CCM ilikuwa ilisita nini kukubali teuzi  alizopata ,akawa ana kula  viapo na kuitumikia SMZ kwa utii na  uaminifu.

'Hata kwa  mtu  anaedaiwa kueneza upekepeke wa CCM haijashinda  uchaguzi aliajiriwa na SMZ ajira  ya daraja la juu ,hakuwahi kuwa  Mjumbe  wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar,si Mkurugenzi  wala Mwenyekiti  wa ZEC " Alisisitiza Mbeto

Hakuna maoni