Zinazobamba

Mbeto: CCM hakishabikii siasa za matabaka , ubaguzi na ukabila

Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejipambanua  si chama cha matabaka ya Ukanda, Udini na Ukabila ndio maana  kilipinga   Siasa za Ubaguzi  wa rangi  huko Afrika Kusini na kuwahifadhi Wapigania Uhuru .

Hivyo basi, kimewaasa watendaji wake ngazi za Matawi, Wadi,Majimbo, Wilaya na Mikoa , kufuata taratibu za kikatiba na kanuni  ili kuendesha chaguzi zilizo Wazi, Huru na za Haki.

Indhari hiyo imetolewa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar  ,Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo  ,Khamis Mbeto  Khamis , alipozumgumza na wanachama pamoja na viongozi wa CCM. 

Mbeto  alisema ni mwiko na marufuku  kwa Kiongozi  au Mwanachama wa CCM , kutumia  lugha  ya ubaguzi ili achaguliwe,  atakaebainika na kuthibitika amefanya hivyo ,matokeo ya ushindi wake yatafutwa .

Alisema kila mwanachama anatakiwa  kufanya kampeni kwa kutumia mbinu halali za kidemokrasia hadi achaguliwe  kwa ridhaa, akitumia ushawishi wake kisiasa , uwezo binafsi  na upeo alionao.

'Hukuna atakaepata  Uongozi  kwa  kutumia lugha ya ubaguzi  aidha  ya ubaguzi wa rangi, ukabila au kwa nasaba . Atakaefanya  hivyo atakiuka  misingi ya maadili na miiko ya chama  .Matokeo ya ushindi wake hatutasita kuyafuta"  Alisema Mbeto.

Aliongeza kusema CCM  ni chama kilichoitangazia dunia  kitapinga  Siasa za Ubaguzi mahali popote  duniani , kimefanya hivyo ikiwemo na  kikivihifadhi  vyama vya wapigania  uhuru  .

"Ardhi yetu  imetumika na kuwa uwanja  mapambano  kwa vyama  vilvyopigania uhuru vilivyopinga  Siasa za  kibaguzi . Tumefanya hivyo kwa kujiamini  , dunia nzima inajua msimamo wa Tanzania chini ya  sera za CCM  "Alisistiza Mbeto. 

Pia aliwakanya wanachama ambao hutegemea uwezo wao kiuchumi  ili kurubuni watu wapiga kura wapate  uongozi  ,wasijisumbue kufanya hivyo kwakuwa hata wakishinda hawatapitishwa na vikao vya juu vya maamuzi.

Akisisitiza zaidi ,Mbeto  alisema fedha kwa CCM  si msingi wa maendeleo, ispokuwa heshima ya mtu mbele ya wenzake itokane na uzalendo  wake, adabu  na uaminifu wake .

"CCM ni chama cha Wakulima na Wafanyakazi. Uongozi si  bidhaa au biashara mtu  akidhani itanunuliwa. Wanachama wetu kataeni kuuza utu na  heshima zenu  kwa kutonunuliwa kama bidhaa sokoni " Alieleza.

Kadhalika  ,Chama Cha Mapinduzi,  hakitaona muhali wala aibu kukata majina yote ya wanachama watakaobanika kutumia  rushwa kwa ajili ya kupata Udiwani, Uwakilishi na Ubunge

No comments