Zinazobamba

VIONGOZI WA DINI WAIOMBA SERIKALI KUUFUTA MTANDAO WA KIJAMII WA "X " (TWITTER) KUTOKANA NA KUHAMASISHA MAPENZI YA JINSIA MOJA.

Na Mussa Augustine.

Viongozi wa Dini nchini wamezitaka Mamlaka za serikali kuufungia mtandao wa Kijamii wa X ambao zamani ulijulikana kama Twitter Kwa kuhamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja (ushoga)

Ombi hilo limetolewa leo Juni 11, 2024 Jijini Dar Es Salaam na Alhaj Dkt Abdul Suleiman wakati akizungumza na waandishi wa habari nakubainisha kwamba  vitendo vya Mapenzi ya Jinsia Moja (Ushoga ) vimepigwa marufuku  hata katika maandiko ya dini ya kiislam na kikristo ,hivyo vitendo hivyo havikubaliki na vinapaswa kulaaniwa mara moja.

Dkt Sule amesema kwamba kufuatia Mtandao wa X ambao hapo zamani ulijulikana kama “Twitter”kuruhusu kuchapisha maudhui yanayohamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ikiwemo ushoga na usagaji Mamlaka zinazohusiana na mawasiliano zinatakiwa kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ikiwemo kufuta  mtandao huo hapa nchini.

Kwa upande wake Askofu na Katibu mkuu wa Kanisa la Methodox Tanzania Allen Siso amesema katika vitabu vya dini vyote havikubaliani na ndoa za jinsia moja akitolea mfano kitabu cha Warumi 1:26 kinachosema 'hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu,hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili,na wanaume nao vivyo hivyo'.

Naye Sheikh Hilal Kipozeo amesema mtandao wa X unatakiwa  kufutwa  haraka iwezekanavyo,nakwamba ni vyema kuundwa  Sheria kali ya Kudhibiti mapenzi ya jinsia moja na usagaji ili kusaidia kizazi kijacho kisiharibike.

“Mungu aliruhusu wanadamu wazaliane na wakaongezeke lakini hili tatizo hata siku moja haliwezi kuruhusu wanadamu wakazaliana na kuongezeka hivyo Mara moja mtandao wa X Ufungiwe"amesema 

Naye mwakilishi wa walimu ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Gongolamboto,Munira Njau amesema kuwa wazazi wamekuwa na tabia za kuwaachia watoto wao wachezee simu zao Hali iliyopelekea watoto kuingia kwenye mitandao hiyo na Kujifunza tabia mbaya siku Hadi siku na hatimaye kuzipeleka mashuleni.

"sisi walimu tunashinda na watoto kuanzia asubuhi mpaka jioni,na tunakutana na wanafunzi ambao tayari Wana viashiria vya tatizo hilo na tunapowahoji wanasema wamekuwa wakisema vimeanzia majumbani na wengine kupitia simu za wazazi wao,hivyo suala hili tuungane wote kusaidia watoto


No comments