Zinazobamba

TCCIA YAISHAURI SERIKALI KUPELEKA NDEGE YA MIZIGO KANDA YA ZIWA

Na Mussa Augustine.

Serikali imeshauriwa kupeleka ndege ya mizigo Mkoani Mwanza ili kurahisisha usafirishaji wa Minofu ya Samaki katika nchi za ulaya.

 Ushauri huo imetolewa Machi 26 ,2024 jijini Dar es salaam na Rais wa Chemba ya Biashara ,Viwanda na Kilimo Tanzania ( TCCIA) Vicent Minja wakati akizungumza na waandishi wa habari kwa ajili ya kutoa tathmini ya ziara iliyofanywa na viongozi wa Chemba hiyo katika Mikoa mbalimbali nakubaini Kuwepo kwa changamoto ya wafanyabiashara wa Minofu ya Samaki kusafirisha kitoe hicho kutoka Mwanza kwenda Nchi za Ulaya.

 Minja amesema kwamba Wafanyabiashara hao wamekuwa wakienda kutumia Usafiri wa ndege katika nchi za jirani ikiwemo Kenya kutokana na na kukosekana kwa ndege ya Mizigo Mkoani Mwanza hivyo ameishauri Wizara ya Uchukuzi kupitia Shirika la Ndege Nchini ATCL kupeleka ndege hiyo ili kurahisisha usafirishaji wa Minofu ya Samaki Nchi za Ulaya.

 Aidha Rais huyo wa TCCIA ameiomba Serikali kupitia Halmashauri zake kuweka Mazingira Mazuri ya usafi katika maeneo ya kuchakata Minofu ya Samaki kwani inahatarisha afya ya Walaji wa Kitoeo hicho.

“Mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Kagera na Mwanza Viwanda vya kuchakata Minofu ya Samaki vinachakata kwa kiwango kidogo sana kwani kuna uhaba wa samaki kuokana na wavuvi kuenda kuuza samakai hao nchi za jirani”Amesema.

 Nakuongeza kuwa “Wafanyabiashara wa Minofu ya Samaki wanapata shida yakusafirisha minofu hiyo nchi za Ulaya kwani hakuna ndege ya Mizigo kutoka Mwanza ,tunaishauri serikali kupitia shirika la Ndege(ATCL)kupeleka ndege ya mizigo ili kurahisisha usafirishaji wa minofu hiyo.

Katika hatua nyingine Minja ameishauri Wizara ya Kilimo kukutana na wakulima wa korosho Mkoani Mtwara ili kujadili Changamoto za mfumo wa stakabadhi gharani pamoja na uuzaji wa mazao yao kwa njia masoko kupitia vyama vya ushirika AMCOS kwani mfumo huo unalalamikiwa na wakulima wa korosho Mkoani Mtwara pamoja na wakulima wa Choroko na Dengu Mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa Rais wa TCCIA Bwana Minja amesema kuwa ziara hiyo imeanza februari 20 , 2024 na inatarajia kukamilika Mei 6 ,2024 katika Mikoa yote nchini,nakwamba kwa Sasa viongozi hao wametembelea Mikoa ya Dar es salaam,Pwani,Lindi,Mtwara,Shinyanga,Geita,Kagera,Mwanza,Simiyu,pamoja na Mara ambapo wamebaini kuwa wafanyabishara wengi wanakumbwa na changamoto mbalimbali.

 "Kuwe na utaratibu mzuri wa Masoko na Stakabadhi gharani ili kuleta manufaa kwa wakulima ,hivyo Serikali ikutane na wakulima izungumze nao kujua changamoto zinazowakabili”Amesema Minja.

 

 

Hakuna maoni