Zinazobamba

PURA wakaribisha wananchi sabasaba, Mradi LNG kuajiri watu 10,000




Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Halfan Ramadhan, akizungumza  na waandishi wa habari hawapo wakati alipotembelea banda ya PURA kwenye wa Maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam

Frank Mwankesi,  akizungumza  na waandishi wa habari hawapo wakati alipotembelea banda ya PURA kwenye wa Maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Halfan Ramadhan, akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi wa Mafuta na Gesi, Robinnancy Mtitu, uzalishaji wa mafuta na gesi wakati wa Maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam.


Tumaini Abdalah akizungumza  na waandishi wa habari wakati alipotembelea banda ya PURA kwenye wa Maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam.

Na Mwandishi wetu

Mwenyekiti wa bodi ya PURA, Halfan Halfani amesema kuwa mradi wa LNG utasaidia kuongeza ajira kwa watanzania ambapo watu takribani elfu kumi wanatarajiwa kupata ajira hizo.


Alisema,kwenye mradi huo wafanyakazi wasiopungua 500, watapata kazi na kwamba katika eneo hilo la mradi kutakuwa na ajira nyingi kwa watu wa bodaboda, mama lishe pamoja na wajasiriamali wengine wa aina mbalimbali

Tanzania inajipanga kuvuna neema ya gesi asilia katika mradi wa kuchakata na kusindika gesi asilia(LNG), mradi ambao kampuni za wazawa  zimepewa fursa ya kunufaika na mradi huo.

Wakizungumza na vyombo vya habari katika maonyesho ya 46 ya biashara ya kimataifa Dar es Salaam (DITF), kwenye banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), baadhi ya Makampuni ya wazawa walisema kuwa wameona thabiti ya serikali katika kuhakikisha wazawa wananufaika kwenye fursa mbalimbali zinazojitokeza katika sekta hiyo ikiwamo mradi wa mkubwa wa LNG.


“Mradi huu wa LNG utakuwa na tija kwa taifa kwani utadumu kwa zaidi ya miaka 50 huku tukitarajia kupata manufaa mara mbili, kwanza hela tutakayopata kwa kuuza gesi ambayo itakuwa ikiuzwa mpaka nje ya nchi na kupata fedha za kigeni na pia kwa kufanikisha nishati  kwa viwanda, nyumba, magari na Taasisi za hapa nyumbani na hivyo kutusaidia kufanya uzalishaji wa ndani” amesema Halfani.


Frank Mwankesi ni Mfanyakazi wa chama cha wafanyakazi cha mafuta na gesi (OGAOGA) ameipongeza serikali kwa kuweka  mazingira wezesha ya ajira katika sekta ya madini na gesi.

Tumaini Abdallah ni mmoja wa vijana wanaofanyakazi kwenye Kampuni za kizalendo zitakazonufaika na mradi wa LNG, ametoa shukrani kwa Pura kwa kuziamini kampuni za ndani za uchimbaji wa gesi na mafuta na hivyo kuaminika kwa Kampuni za kigeni zinazokuja kutekeleza uchimbaji  wa gesi asilia mkoani Lindi.

Tumaini ametoa wito kwa Vijana wa Kitanzania kujitokeza kwa wingi kwenye fursa hiyo kwa kuwa serikali ipo tayari kuwapa nafasi.

“Vijana msiogope msaada upo na serikai ipo kwa ajiri yetu kama ambavyo sisi tumenufaika kwenye mradi huu,"anasema Tumaini

ENDS, 

No comments