Zinazobamba

FCC yawakaribisha wananchi sabasaba kupata elimu

 

Mkurugenzi Uendeshaji wa Tume ya Ushindani (FCC ) Godfrey Machimu akiwajibika katika banda la FCC sabasaba, Machumu alisema Tume hiyo imejipanga kutoa elimu kuhusu shughuli mbalimbali wanazozifanya.
Afisa Uchunguzi wa FCC Waambie Malata  akiwa katika banda  tayari kwa majukumu yake, FCC imeweka banda lao katika ukumbi wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara.

Afisa Kumlinda Mlaji katika Tume ya Ushindani Amina Mjungu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu majukumu ya tume hiyo.



Na Mwandishi wetu

TUME ya Ushindani (FCC) imewshauri wananchi kupeleka malalamiko yao yanayohusiana na changamoto za kibishara ili waweze kupata haki yao ya msingi.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa uendeshaji wa Tume ya ushindani, Godrfrey Machimu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa, yanayoendelea viwanja vya Mwl. Nyerere Dar es Salaam.

Tume ya ushindani imepiga kambi sabasaba ikiendelea kutoa elimu huku ikiwataka wanaofika kwenye maonesho hayo kufika kwenye banda lao lililopo katika Banda la Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara ili kupatiwa elimu

Alisema wamejipanga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu shughuli wanazofanya kwa kutumia Sheria ya Ushindani na Sheria ya Alama za bidhaa.

Tuko hapa tangu Juni 28 mwaka huu tukitoa elimu kwa wananchi ili waifahamu FCC na shughuli zake, tunapenda kushukuru kwa muitikio mkubwa ambao umejitokeza kuja kupata elimu, kuielewa FCC na kujua inafanya nini kwa kupitia sheria zake mbili kwa maana ya Sheria ya Ushindani na ile Sheria ya Alama za bidhaa.



“Karibuni muweze kuendelea kujifunza FCC tunafanya nini katika upande mzima wa kudhibiti bidhaa bandia, tunafanya nini katika suala zima la ushindani, tunafanya nini katika kuwezesha biashara na uwekezaji,”amesema

FCC kama taasisi wezeshi wanasaidia watu wenye mitaji yao ikiwamo wafanyabiashara wakubwa wanaotaka kuwekeza nchini. 

“Pia kama mteja ana biashara yake amesajili nembo yake italindwa na FCC, lakini kama kuna kampuni yake anafikiria haifanyi vizuri na angependa kujiunga na kampuni nyingine FCC iko tayari kwa ajili ya kuichunguza na kuangalia kama muunganiko huo hauna madhara katika ushindani,”


“Kama kuna biashara unafanya katika soko lakini kuna mshindani mwenzako anakufanyia miendeno isiyokubalika kwa mujibu wa sheria, FCC iko tayari kwa ajili ya kufanya uchunguzi na kutoa adhabu iwapo mfanyabiashara atabainika anakinzana na sheria ya ushindani.


“Kwa hiyo tuko hapa kwa ajili ya kuwezesha biashara, tuko hapa kwa ajili ya kulinda biashara lakini tuko kwa ajili ya kumlinda mtumiaji.

Naye Afisa uchunguzi wa FCC alisema Sheria ya Ushindani namba Nane ya mwaka 2003 inakataza mambo makubwa matatu. Moja ni makubaliano baina ya washindani yanayokiuka ushindani.

“Baadhi ya mambo hayo ni kama makubaliano baina ya washindani kupanga bei, washindani kupunguza uzalishaji au usambazaji wa bidhaa au huduma lakini pia inakataza makubaliano baina ya washindani kupanga njama kwenye zabuni

“Jambo la pili ambalo linakatwaza na Sheria ya Ushindani ni matumizi mabaya ya nguvu ya soko kuwa na nguvu ya soko sokoni kwa wafanyabiashara ni jambo jema na ni ishara ya kuimarika kwa biashara lakini namna nguvu hiyo inavyotumika inaweza ikasababisha uvunjifu wa sheria ya ushindani.

“Kwa mfano pale ambapo mfanyabiashara mwenye nvuvu sokoni akawa anatumia nguvu hiyo kukataa kutoa huduma au bidhaa kwenye baadhi ya sehemu au kwa baadhi wafanyabiashara, hilo ni kosa kwa mujibu sheria ushindani namba Nane.

Lakin mfanyabishara mwenye nguvu sokoni anazuiliwa na sheria ya ushindani kutumia nguvu yake hiyo pale,”amesema.

Aidha ametoa mfano akiwa yeye ndio msambazaji au muuzaji wa malighafi ambayo inatumika kutengeneza bidhaa fulani halafu akawa anawanyima malighafi hiyo kwenda kutengeneza bidhaa hilo ni kosa kwani atakuwa anatumia nguvu yake vibaya, nguvu ya soko vibaya.

Amesema lingine linalokatazwa na Sheria ya Ushindani ni miungano ya kampuni ambazo zinatengeneza au kuimarisha hodhi ya soko, kwa mujibu wa sheria ya ushindani inataka kampuni ambazo zinataka kuungana na thamani yao inafikia bilioni 3.5 zinawajibika kutoa taarifa mbele ya FCC kabla hazijaungana ili waweze kufanya uchambuzi wa kisheria na kiuchumi kuona kama muungano huo au kununuana kwao hakutakuwa na madhara ya kisheria au kiuchumi

Wakati huo huo Afisa Kumlinda Mlaji katika Tume ya Ushindani Amina Mjungu ameeleza jukumu mojawapo la tume hiyo ni kumlinda mlaji kuhusu huduma na bidhaa anayoipata sokoni huku akifafanua mlaji ni mtumiaji wa mwisho kabisa wa huduma na bidhaa.

“Katika kumlinda mlaji Tume ya Ushindani inapokea malalamiko ya walaji na kuyapitia na kuyatatua ili kumaliza mgogoro husika.Pia inapokea mikataba ya walaji inayoandaliwa na upande mmoja , mikataba ile inapitiwa katika Tume ya Ushindani na kuhakikisha vile vigezo na masharti vinakidhi viwango kwa pande zote za mlaji na mtoa huduma.

“Hivyo tunawahimiza watoa huduma walete mikataba yao ili tuweze kuisajili katika Tume ya Ushindani kabla ya kutumika sokoni na watumiaji sokoni ambao wamepatiwa huduma ambazo hazipendezi tume inapokea malalamiko yao kupitia ofisi iliyopo Dar es Salaam au Dodoma.Pia wanaweza kuwasiliana nasi kwa namba ya kupiga bure ni 0800110094.

 

No comments