Mamia ya wananchi wafurika Banda la PURA sabasaba
Na
Mwandishai wetu
Viongozi
mbalimbali kutoka Taasisi tofauti katika sekta ya mafuta na gesi wameungana na
mamia ya washiriki wa maonyesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba) kuhudhuria
banda la PURA kujifunza na kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Taasisi
hiyo.
Baadhi
ya viongozi wa ngazi za juu waliotembelea banda hilo na kujifunza ni pamoja na Mkugrugenzi Mtendaji wa Shirika
la Mafuta Tanzania (TPDC) Dr. James Mataragio Pamoja na Makamu wa Rais wa Shell Exploration & Production
Tanzania Ltd Bw. Jared Kuehl.
Viongozi hao warikaribisha na Mkurugenzi Mkuu wa PURA Injinia.
Charles Sangweni ambaye alieleza kuwa dhumuni la kushiriki kwenye maonesho hayo
ni kutoa elimu kwa umma kuhusu suala la Mafuta na gesi pamoja na fursa
zinazopatikana kwenye sekta hiyo.
"Tumeshiriki
kwenye maonesho haya kwa sababu ya kutoa elimu kwa watanzania kuhusu PURA, Kazi
zake, fursa zilizopo katika sekta na jinsi ya kuzitumia ili kujiletea
maendeleo,” alisema
Injinia.
Sangweni alitumia fursa hiyo kueleza kuhusu mradi wa LNG, hasa fursa zilizopo
mara tu utakapoanza kufanya kazi.
Alisema
Ujenzi wa LNG unatarajia kuanza rasmi mwaka 2025, na katika kipindi hicho mradi
unatarajiwa kutengeneza ajira 10,000 pamoja na ajira za moja kwa moja 600
"Katika
kipindi cha utekelezaji wa mradi pia kutakuwa na fursa mbalimbali ikiwamo ya
kuuza huduma na bidhaa, mradi unafaida kubwa kwa umma,” aliongeza
Thamani
ya mradi wa LNG unaelezwa kufikia Dola 30 Bilion sawa na Shilingi za Kitanzania
Trilioni 72, unatarajiwa kuzalisha gasi kwa kipindi cha miaka 30

No comments
Post a Comment