Zinazobamba

NIDA wajipanga kuboresha vitambulisho vinavyokwisha muda wake

 




Msemaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ( NIDA), Geofrey Tengeneza  amesema wako mbioni kuanza zoezi la kuhuisha taarifa za vitambulisho vilivyotolewa mwaka 2012 ambavyo sasa vinaonekana vimepita muda wake

 

Aidha Tengenza aliwatoa hofu Watanzania juu ya kupata usumbufu wa foleni kutokana na zoezi hilo linalotarajiwa kuanza hivi karibuni kwani kitu kikubwa wanachoangalia ni upigaji wa picha, zoezi ambalo halichukui muda mrefu.

 

 

“Vitambulisho vya Taifa vya mwaka 2012  vinaonesha kuisha muda wake, watu hawatakiwi kuwa na hofu, tutavihuisha vitambulisho vyao, pia alwataka kuendelea kutumia vitambulisho hivyo kwani utambulisho wao utabaki palepale.



Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 46 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, alisema kinachokwenda kuisha muda wa matumizi ni kibebeo cha kitambulisho lakini utambulisho wa mwanachama unabaki palepale.



Alisema huduma zote ambazo wamekuwa wakizipata kupitia kitambulisho hicho au namba ya kitambulisho utabaki kuwa palepale licha ya muda wa kitambulisho kwenda kuisha.



"Licha ya kwenda kuisha kwa muda wa matumizi ya kibebeo cha kitambulisho cha taifa naomba Wananchi mjue kuwa utambulisho wa mwananchi unapaki pale pale na auishi muda wa matumizi"alisema



Tengeneza alisema kinachokwenda kufanyika baada ya muda kuisha muda wa kitambulisho mwananchi atapaswa kwenda katika ofisi ya wilaya katika eneo ambalo anaishi kufika pale kwa ajili ya kupigwa picha.



"Zoezi ambalo litafanyika ni kupiga picha tu hakutakuwa na hatua uhakiki wa taarifa zako na baada ya hapo NIDA tutaendelea utaratibu wa kuandaa kanzi data yetu"alisema



Aliendelea kufafanua kuwa matumizi ya kitambulisho cha taifa yamekuwa ni ya miaka 10 lengo likiwa ni kufanya mabadiliko ya taarifa za Wananchi tofauti na zile ambazo alitoa awali.



Akitaja sababu za kufanya mabadiliko ndani ya miaka 10 Tengeneza alisema inawezekana mtu akawa amebadilisha makazi ya awali hivyo ni lazima  taarifa zake zikahuishwa katika mfumo wa kanzi data.



Pia alisema katika muda wa miaka 10 muonekano wa mtu unaweza ukawa umebadilika hivyo katika kipindi hiki ni lazima afanye mabadiliko.



"Hizi ndizo sababu ambazo kwanini tumeweka muda wa miaka 10 nawaomba watanzania wasiwe na hofu yoyote Wala kuhusu foleni pindi mchakato utakapoanza wa kupiga picha hakutakuwa na foleni ya aina yoyote endapo hatakuwa na taarifa za kuhusisha"alisema



Vilevile alisema vitambulisho hivyo ambavyo ni vya mwaka 2012 avitakuwa vikiisha muda mmoja na badala yake vinaisha kwa muda tofauti kulingana na tarehe na mwezi na mwaka hivyo Wananchi wasiwe na hofu kuhusu suala la foleni.



Aidha alisema NIDA imejipanga kutoa huduma hiyo kwani tayari imekwisha toa oda ya vifaa vipya kwa ajili ya zoezi hilo.

 

No comments