UCSAF yatekeleza miradi katika kata 829 kati ya kata 1,234 zilizo ainishwa na mfuko
| Afisa mawasiliano wa mfuko wa UCSAF Bi. Celina Mwakabwale akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonesho ya sabasaba, jana |
Mfuko wa
mawasiliano kwa wote (UCSAF) umetoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanalinda
miundombinu ya mawasiliano hasa minara ambayo imekuwa ikijengwa karibu na kata
zao.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika maonesho ya 46 ya biashara ya kimataifa (sabasaba),
Afisa mawasiliano wa mfuko huo Bi. Celina Mwakabwale alisema mawasiliano ni
muhimu sana katika maisha ya mtu.
“Ukitaka
kujua kuwa mawasiliano ni maisha, jaribu kuzima siku yako leo, hivyo ni vizuri
watu wakatambua kuwa kuharibu miundombinu kunapelekea kukatika kwa mawasiliano,”
alisema
“Kuna
wakati watu wenye nia ovu wanafanya kazi ya kuhujumu miundombinu wakidhani kuwa
haiwahusu, miradi ile inawahusu kwa sababu kuna sehemu ya kodi yao imetumika
kujenga minara,” alisema
“Mawasiliano
yanaokoa maisha, kuna wakati unaweza kuwa na mgonjwa nyumbani, kama hauna simu
hutaweza kumsaidia kwa haraka mgonjwa,” aliongeza
Aidha akizungumzia
ujio wao katika maonyesho ya sabasaba, Mtaalam huyo wa masuala ya mawasiliano
alisema lengo lao ni kuhamasisha na kutoa elimu juu ya huduma wanazotoa.
Alisema Mfuko
huo unafanya kazi kubwa ya kujenga minara katika maeneno ambayo hayana huduma
na ipo lakini ni hafifu.
Aliongeza kusema
mfuko wa Yuksaf umelenga kuleta mapinduzi katika sekta ya mawasiliano kwa umma,
tunalenga Zaidi katika maeneno ya pembezoni.
Hapa tumekuja
kutoa elimu kwa umma, lengo wafahamu sisi Yuksaf ni watu gani na tunafanya nini
katika kazi zetu.
“Hapa tunapokea
maoni mbalimbali kuhusu changamoto za mawasiliano katika maeneo wanapotoka,
tuko tayari kwa ajili ya kuwahudumia, tunawashauri wananchi waje sabasaba
kupata taarifa Zaidi juu ya kazi zinazofanywa na UCSAF, tunao wataalam wa
ktosha ambao watawahudumia.
Akizungumzia
kuhusu miradi, alisema wanayo miradi mingi ambayo inaendelea ikiwemo mradi wa
kufikisha mawasiliano katika maeneno mbalimbali
“Miradi inayotekelezwa
ni pamoja na huduma za mawasiliano ya simu, mfuko unafikisha huduma za
mawasiliano ya simu katika maeneno yasiyo na huduma hiyo na yenye mawasiliano
hafifu, mpaka kufikia April, 2022 mfuko umetekeleza miradi katika kata 829 kati
ya kata 1,234 zilizoainishwa na mfuko,” alisema
Aidha kwenye
kuboresha usikivu wa redio,Celina alisema kwa sasa mfuko unatekeleza mradi wa
kuboresha usikivu wa redio ya taifa na redio ya kijamii katika baadhi ya maeneo
ya nchi hasa mipakani.
Alisema wamekuwa
wakiboresha usikivu wa redio hasa maeneno ambayo usikivu wake ni hafifu lakini
pia wamekuwa wakijenga minara katika maeneno ambayo redio haijafika.
Mtaalam huyo
alisema kwa kushirikiana na TBC, mfuko umeweza kukamilisha ujenzi wa studio za
redo za jamii Dodoma na Arusha pamoja na vituo vya kurushia matangazo ya radio
TBC Taifa na TBC FM.
Vituo hivyo
vimejengwa kisaki na mrimba Mkoani Morogoro, Ngara Mkoani Kagera, Ruangwa
Mkoani Lindi na Ludewa Mkoani Njombe.
Mbali na
mafanikio hayo pia alisema mfuko umefanikiwa kujenga kituo cha miito ya dharura
Zanzibar lengo ni kuiwezesha serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa na kituo cha
kuratibu taarifa za matukio ya dharura.
Baadhi ya
matukio hayo ni pamoja na Moto, ajali, mlipukowa magonjwa mbalimbali, tayari kituo
hicho kimeshakamilika na kuzinduliwa, wakazi wa Zanzibar wameanza kunufaika nacho
kwa kupiga simu ya bure kupitia nambari 190.
Vilevile alisema
Mfuko huo kupitia mradi wa kuunganisha shule kwenye intaneti, umekuwa
ukizipatia shule za umma vifaa vya TEHAMA na kuziunganisha na mtandao wa intaneti
kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kujifunza kupitia vifaa hivyo katika hatua
za awali.
Mpaka sasa
jumla ya shule 811 zimepatiwa vifaa ikiwemo Kompyuta na prita.
Alisema,
pia upo mradi wa tiba Mtandao, ambao umelenga kuunganisha hospitali kadhaa na
Hospiatali ya Taifa ya Muhimbi (MNH)na Taasisi ya Mifupa MOI ili kuboresha
utoaji wa huduma za afya katika hospitali zote zilizounganishwa kwa kuwawezesha
wananchi kupata huduma za madaktari
Kimsingi Mfuko
wa mawasiliano kwa wote (UCSAF) ulianzishwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa sheria ya Bunge nambari 11 ya mwaka 2006 sura ya 422 kwa lengo
la kupeleka na kufanikisha huduma ya mawasiliano kwa wananchi waishio katika
maeneno machache ya mijini na maeneno mengi ya vijijini ambayo hayana mvuto wa
kibiashara kwa watoa huduma za mawasiliano.
Mwaka 2009
kanuni za kuhuisha Mfuko zilipitishwa na Mfuko kuanza kazi Julai 1, 2009.
Dhamira ya
mfuko huu ni kuratibu upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini na maeneno
ya mijini yenye mawasiliano hafifu kwa kushirikiana na wadau wengine wa sekta
ya mawasiliano, lengo ni kufikia maendeleo ya kiuchumi na kijamii sambamba na
dira ya maendeleo ya Tanzania ifikapo 2025.
Dira ya
mfuko huu ni kufanikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano Tanznia
kikamilifu na kwa usawa.
Post Comment
No comments
Post a Comment