Mwenyekiti Bakwata agawa futari kwa makundi maalum dar
Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti wa Halmashauri Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA),
Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Hussein Afif Al Azhary amegawa futari kwa familia
150 za makundi maalum yakiwemo walemavu wa macho na viziwi.
Akizungumza
na waandishi wa habari waliohudhuria katika zoezi hilo, Sheikh Afif alisema
wameweza kugawa futari kwa familia 70 za walemavu wa macho.
Aidha
kwa upande wa viziwi, Sheikh Afif alisema wamefanikiwa kukabidhi futari kwa
familia 80 na kufanya jumla ya wanufaika kuwa 150.
“Kila
kifurushi kimoja kina mafuta ya kula lita 3, maharagwe, ngano, mchele, ofisi
yangu imeratibu jambo hili na limekwenda vizuri kila mtu amefurahi,” alisema
Afif.
Sheikh
Afif ambaye ni muhitimu wa Chuo Kikuu cha Al-azhar cha Jijini Cairo, Misri
mwaka 2013 alisema wahisani wamefurahishwa na ugawaji wa futari na kuahidi
kuendelea kutoa misaada hiyo siku za usoni.
Kwa
upande wao wanufaika wa futari hiyo, wameshukuru kupatiwa msaada na kuwaomba
wadau wengine kutoa ili wapate fadhila za Allah
Sheikh
Afif amedhamiria kuleta mabadiliko katika jiji la Dar es salaam hasa kulifanya
baraza la mkoa kufahamika vizuri katika sekta za elimu, uchumi na afya.
Hapo
awali Mkoa wa Dar es salaam ulionekana kumezwa na ofisi ya Makao Makuu ya
Bakwata kiasi kwamba waislamu wanashindwa kutofautisha vitu vya baraza la mkoa
na vile vya makao makuu.
Sheikh
Afif ambaye ndiye Mwenyekiti mdogo kuliko wote wa kuchaguliwa, akiwa na miaka
35, alisema ofisi yake inafanya kila linalowezekana kuwaletea mabadiliko
waislamu wa Dar es salaam, jiji lenye waislamu wengi.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni