Zinazobamba

MKINGA: WANAOEGESHA MAGARI WALIPE USHURU KWA WAKATI WAEPUKE USUMBUFU



Meneja wa Tarura Mkoa wa Dar es salaam Geofrey Mkinga akizungumza na mwandishi wa mtandao huu (hayupo pichani) wakati wa mahojiano maalumu ofisini kwake.

Na Mussa Augustine

Mamlaka ya Usimamizi wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Dar es salaam  imewataka wamiliki wa magari kujisajili kwenye mfumo mpya wa kieletroniki ulioanzishwa na rasmi na mamlaka hiyo kwa ajili ya kuwasaidia kulipa ushuru wa maegesho kwa kutumia njia ya mdandao wa simu za mkononi.

Mamlaka hiyo pia imewataka wamiliki wa magari wanaoingia maeneo ya katikati ya jiji la Dar es salaam walipe ushuru wa maegesho kwa wakati ili kuepkana na usumbufu unaoweza kujitokeza .

Rai hiyo imetolewa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es salaam Geofrey Mkinga wakati akifanya mahojiano maalumu na Mtandao huu ofisisni kwake ambapo amebainisha kwamba mfumo wa kielektroniki wa ”TeRMIS APP” ulioanzishwa na Mamlaka hiyo umelenga kudhibiti upotevu wa mapato ya serikali lakini pia unamsaidia mteja kuondokana na usumbufu unaojitokeza wa kulipa ushuru wa maegesho kwa kupitia risiti za kawaida.

Aidha Meneja Mkinga amesema kwamba wateja ambao wanafanyabiashara zao kwa muda mrefu akitolea mfano masaa kumi au zaidi kwa siku nivyema walipie kifurushi cha shilingi 2500 cha siku nzima kwani kufanya hivyo inasaidia kulipa gharama kidogo ukilinganisha na kulipa shilingi 500 kwa saa moja ambapo inakuwa gharama kubwa zaidi.

Amesema kwamba mteja atakaecheleawa kulipa ushuru anaodaiwa atatozwa faini ya shilingi elfu kumi ndani ya siku 14,na kadri atakavyochelewa kulipa deni lake faini hiyo itaendelea kuongezeka, hivyo wanaoegesha magari maeneo mbalimbali wanapaswa kulipa ushuru wa maegesho kwa wakati ili kuepuka usumbufu.

“Kila baada ya siku 14 endapo mteja ambaye amejisajili kwenye mfumo atakua hajalipa ushuru wa maegesho anaodaiwa basi faini yake itaanza kuhesabika na endapo ataendelea kukaidi kulipa atafikishwa kwenye vyombo vya Sheria kwa ajili ya hatua zingine ambapo anaweza  kufungwa jela mwaka mmoja na kulipa faini pia kulipa deni lote analodaiwa “amesema Mkinga

Nakuongeza kuwa “Nia ya serikali yakuongeza muda kutoka siku 7 hadi 14 isiwafanye wateja wanaodaiwa ushuru wa maegesho isiwapelekee usumbufu hivyo watu wasitegemeee kuulizwa na hakutakuwa  majadiliano yoyote ya ana kwa ana na mtoza ushuru,zoezi la kulipa kwa njia ya mtandao limeanza rasmi Machi  mosi mwaka huu.

Aidha sambamba na hayo Meneja huyo amesema hatua za kuboresha mfumo huo zimefanikiwa kwa asilimia 98 na TARURA bado inaendelea kuomba ushirikiano kwa wadau mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi ya mfumo huo.

Amesema mfumo wa kielektroniki wa kukusanya ushuru wa maegesho ulianzishwa rasmi Mwezi Septemba Mwaka jana ,lakini ulibainika kuwa na changamoto kadhaa ambazo baadhi ya wateja walianza kuzilalamiki hata hivyo mwezi  Oktoba 2021 serikali  ilichukua hatua yakusitisha kwa muda matumizi ya mfumo huo ili kuufanyia marekebisho.

Mwezi Machi Mwaka huu Mfumo huo umeanza rasmi kutumika baada ya kufanyiwa marekebisho makubwa ambapo changamoto zilizokua zimebainika ni pamoja na kukosekana kwa elimu yakutosha juu ya matumizi ya mfumo huo,pili wateja walioegesha magari kushindwa kufahamu wapi waliegesha magari yao,huku changamoto nyingine ikiwa ni kukosekana kwa taarifa zao za maegesho (Notefication) ambapo changamoto hizo tayari zimefanyiwa ufumbuzi.

No comments