VIONGOZI NA WANANCHI WA KATA YA MAJOHE WAFURAHISHWA NA BUNGE LA JAMII LILILOFAYIKA KATIKA KATA YAO.
TGNP kwa kushirikiana na kituo cha Taarifa na Maarifa kata ya Majohe wametakiwa kuwa na Bunge endelevu la jamii, ili kuweza kuibua changamoto na kufahamishana mambo mengi yakimaendeleo katika kata hiyo kati ya viongozi na wanachi wao.
Diwani wa kata ya Majohe Mh. Mohamed Sangonde Akitoa majibu kwa wananchi wake mapema jana katika bunge la jamii lililofanyika kata Majohe jijini Dar es salaam. |
Hayo yameelezwa
na Diwani wa kata ya Majohe Mh. Mohamed Sangonde
mapema jana Disemba 31, 2021 katika Bunge la jamii lililofanyika katika kata hiyo likiwakutanisha
viongozi wa kata, mitaa Pamoja na wananchi wao ili kuweza kupena elimu na
taarifa mbalimbali za kimaendeleo katika kata hiyo.
Diwani huyo
amesema kuwa amefurahishwa sana na Bunge hilo lililofanyika katika kata yake kwani
limekuwa ni Jukwaa zuri la kuwakutanisha wanachi na viongozi wao na kuweza
kuhoji mambo mbalimbali katika kata yao na viongozi kuweza kutoa majibu ya moja
kwa moja kwa wananchi wao.
Aidha diwani
huyo amesema kuwa mpaka sasa kata ya Majohe imepata fedha takribani shilingi Milion miambili na hamsini ( 250,000,000/= ) kwa ajili ya ujenzi wa zahanati katika kata hiyo.
Ameendelea kwa
kusema kuwa wanamshukuru Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwani wampatiwa madarasa
kumi katika kata hiyo ambapo mpaka kufikia tarehe 17 januari 2022 madarasa hayo
yataanza kutumika, Kwani ujenzi wake utakuwa umekamilika kwa asilimia mia ikiwa tayari mpaka madawati kwa
ajili ya wanafunzi watakao fanya vizuri katika mtihani wa darasa la saba.
Mwenyekiti wa kituo cha Taarifa na Maarifa kata ya Majohe Bi. Amina Nassoro akiwakaribisha wageni katika Bunge la jamii mapema jana jijini Dar es salaam. |
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa kituo cha Taarifa na Maarifa kata ya Majohe Bi. Amina Nassoro
amesema kuwa wao kama waandaaji wa Bunge hilo wameweza kuwaalika wananchi
kutoka mitaa yote ya kata ya Majohe ikiwemo mtaa wa Kichangani, Viwege, Rada, Mji
mpya Pamoja na Kivule.
Ameongeza kuwa
mpaka kuleta bunge mtaani hapo walianza na kufanya utafiti mdogo kwa wananchi
kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu kama kushiriki katika mikutano ya kuibua ya serikali
za mitaa, kuhusu mipango mbalimbali ya serikali ikiwemo MTAKUWA na imeonekana wananchi wengi hawashiriki na hata hizi
kamati mbalimbali za mitaa yao hawazijui kabisa.
Ameendelea kusema
kuwa wamepata Faraja kubwa kwani wananchi wameweza kupata majibu sahihi ya
maswali yao kupitia viongozi wao, lakini wameelekezwa ni wapi mahali sahihi pa
kupeleka malalamiko yao Pamoja na kesi mbalimbali za ukatili wanazokutana nazo
huko katika mitaa yao.
Kwa upande
wake mkazi wa kata hiyo Bw. Abdul Kasembe amesisitiza kuwepo na nguvu ya Pamoja kwa
viongozi Pamoja na wananchi wao, kwani hii itasaidia kupata utatuzi wa
changamoto kwa wakati endapo kutakuwa na ushirikiano kwa maana kiongozi peke
yake hawezi kumaliza matatizo yote bila kushirikisha wananchi wake.
Naye Tabu Ally mkazi wa kata hiyo ameonyesha mfano wa nguvu za Pamoja kwa kushirikiana na wananchi wenzake wameweza kununua magogo na kujenga kivuko cha muda wakati wakisubiri diwani atakapoleta karavati aliloahidi wakati wa kampeni.
PICHA ZA MATUKIO...
No comments
Post a Comment