Zinazobamba

WANASEMINA ZA GDSS WAFANYA UCHAMBUZI WA TAARIFA YA MAPATO KATIKA SEKTA YA MADINI.

Baadhi ya sheria zetu za madini zinahitajika kufanyiwa maboresho kama siyo kusukwa upya kwani zimekuwa zikiwanufaisha sana wawekezaji ambao wengi ni wageni kuliko wazawa.

Afisa Programu Mwandami wa TGNP. Joyce Mkina akiwaongoza wanajamii kujadili sekta ya madini nchini. 

Hayo yameelezwa mapema jana Septemba 22, 2021 na Afisa programu mwandami wa TGNP Bi. Joyce Mkina katika semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS), ambapo ameshirikiana na wanajamii kutoka kata mbalimbali za jiji la Dar es salaam kufanya uchambuzi wa taarifa za Mapato kupitia Sekta ya Madini.

Amesema kuwa sheria hii kuna baadhi ya vipengele vimeshindwa kumuwajibisha muwekezaji moja kwa moja, kwa mfano kipengele kinachosema muwekezaji anapaswa kuboresha makazi au kuanzisha makazi mapya kwa wale anaotaka kuwaondoa katika eneo husika sheria haijasema ni kwa muda gani anapaswa kufanya hivyo.

“Sheria hii haitoi ufafanuzi wa moja kwa moja inaposema kuboresha makazi bila kumpa muda maalum na ndio inakuja kuwa mtu amekaa miaka kadhaa anakwambia ajapata chochote kama hakupata sasa miaka yote hiyo alikaa kufanya nini, na inatokea mpaka anaondoka bila kufanya chochote na kampuni inabadilishwa jina huu ndio mchezo wanaotuchezeaga hawa wawekezaji” Amesema Joyce

Kwa upande wake Mtenganda Hosein mkazi wa kata ya Mabibo amesema kwa yeye angependa sheria hii ingweza kuwakutanisha wahusika moja kwa moja kujadiliana kati ya mwenye eneo na muwekezaji ili waweze kufanyiana tathmini ya kiwango sahihi cha kulipana.

Naye Rhoda Mdoe mkazi wa Mburahati ameitaka serikali na taasisi binafsi kuweza kupeleka elimu kwa wakazi wa maeneo ya karibu na migodi kwani hii itaweza kuwasaida kufahamu haki na madai yao kwa muwekezaji.

Mmoja wa wachangiaj Bw. Kennedy Macher amsema kwa upande wake ameona ingependeza Zaidi kwa yule ambae eneo lake litabainika kuwa na madini basin a yeye apewe hisa katika kampuni hiyo itakayokuwa ikichimba madini hayo.

Na mwisho angetamani pia kuona wakazi wanaoishi karibu au kuuzunguka mgodi huo kupewa nafasi ya kwanza katika kupatiwa ajira kwani hii itasaidia wakazi wa eneo husika kunufaika na uwepo wa mgodi huo.

Afisa Programu Mwandami wa TGNP. Joyce Mkina akitoa ufafanuzi wa jambo fulani, mbele ya wanajamii ambao hawapo pichani.
Baadhi ya washiriki wa semina wakifuatilia mafunzo kwa umakini.

Afisa program wa TGNP, Frola Kamamy  akichangia mada katika semina ya GDSS.
Mshiriki wa semina za GDSS Mwajuma Abdul akichangia mada katika semina ya wiki hii, juu ya uchambuzi wa mapato yatokanayo na sekta ya madini.

Baadhi ya washiriki wakifuatlia mafunzo.
Mafunzo yakiendelea.











Hakuna maoni