Zinazobamba

Andalusia waja na kongamano la ndoa, Mufti Mgeni rasmi






Mwandishi wetu

Mufti na Sheikh Mkuu waTanzania Sheikh Abubakar Zubeir anatarajiwa kuongoza jopo la masheikh wa Jiji la Dar es salaam na Viunga vyake katika kongamano maalum la wanandoa lililoandaliwa na kituo cha mafunzo cha ANDALUSIA linalotarajiwa kufanyika Septemba 26, 2021 katika ukumbi wa DYCCC uliopo Chang’ombe Jijini Dar es salaam.

 

Kwa mujibu wa mwanakamati ya maandalizi ya kongamano hilo, Akhy Said Salim Khamis, amesema Mufti atafungua kongamano hilo na kuzindua kozi rasmi ya mafunzo ya ndoa(fiqhi ya ndoa) inayotarajiwa kufanyika kila maeneo inshaa allaah.

 

Aidha amewataja walimu wanaotarajiwa kutoa mada kuwa ni pamoja na Sheikh Muhammad Iddi (Abuu Iddi) ambaye ataeleza MAKOSA YANAYOFANYIKA KABLA NA BAADA YA NDOA, lakini pia atakuwepo Sheikh Muharami Mziwanda ambaye atazungumza mada NINI MAANA YA NDOA?

Wengine ni Sheikh Othman Khamis, Imam wa msikiti wa Mtoro ataezungumzia mada ya VIPI TUTAWEZA KUZITUNZA NDOA ZETU pamoja Sheikh Abdulrahman Muhina maarufu baba Kiruwasha(babie sheghele)ambae atawasilisha mada: UTAMU KATIKA MAISHA YA NDOA MAMBO NI HUKU NA HUKU ambao wamejianda vilivyo kufikisha daa’wah kwa wataohudhuria.

 

Amewashauri waislam na wasio waislam kuchachangamkia fursa kusiriki kongamano hilo na kujiunga na mafunzo ya kufahamu ndoa kiujumla,kwani itasaidia kuimarisha ndoa ambazo zinalegalega lakini pia kukinga ndoa za wapendanao wanaotaraji kuingia ndoani.

Said Salim Khamis albakry ambaye pia ni Mudir(Mwalim Mkuu) wa Madrasat IHSAANIYYAH (tandale) amesema: mafunzo hayo yatatolewa kwa kushirikiana na Baraza kuu la waislamu Bakwata na wameweka kiingilio cha shilingi elfu kumi na tano 15000/kwa ajili ya kuchangia gharama za uandaaji pamoja na chakula kwa washiriki wote pamoja na vinywaji.

Aidha akizungumzia kwanini wamekuja na kongamano hilo,Akhy Said salim alisema: "kwa sasa kumekuwa na tatizo kubwa la ndoa nyingi kuvunjika jambo ambalo ni kinyume na maisha walioishi wazazi wetu".

Alisema wazee wa zamani walifanikiwa kuishi pamoja hadi uzeeni,waliweza kuzikana lakini vijana wa sasa wameshindwa kufikia mafanikio hayo huku chanzo kikubwa kikitajwa kuwa ni ukosefu wa elimu ya ndoa.

Ameongeza kusema ndoa nyingi zimekuwa ni kaa la moto,wengine wamekuwa wakiishi kwa mazoea au pengine kuogopa kuwatesa watoto jambo ambalo wamebaki hawana amani ya ndoa bali wanaishi kama wapo katika gereza.

“Changamoto iliyopo sasa katika jamii ni kukosa mafunzo ya ndoa,ikiwa leo mtu akitaka kufuga lazima akasomee kozi ya ufugaji,mtu akitaka kuendesha gari lazima akasomee kozi ya udereva vile vile mtu akitaka kuswali lazima asome Fiqih za swala, vipi kuhusu elimu ya ndoa? ndoa ambayo ni maisha ya kudumu kwa watu.

Kubwa ambalo limeondoka kwetu ni kukosa mafunzo thabiti ya ndoa,ukiangalia hata katika mitandao ya kijamii,meza za masheikh,hata kwenye maofisi ya serikali kuna mmomonyoko wa maadiili,sababu kubwa ni kukosa elimu sahihi ya mafunzo ya ndoa.

 

Sisi ANDALUSIA kwa kushirikiana na Baraza la waislam Tanzania (Bakwata) chini ya usimamizi wa samaha mufti sheikh ABUUBAKAR ZUBEIR tumeona ni vizuri kuandaa semina ili kusaidia kuponya ndoa nyingi lakini pia kuwa kinga kwa wanandoa wapya na wanaotarajia kuingia katika ndoa,” alisema Mwenyekiti wa kitengo cha wanawake Khadija Ali Alwi.

 

Kwa upande wake Imam wa msikiti wa Mtoro, Sheikh Othman Khamis amekiri kuwa atakuwepo siku ya tukio na kuwaomba waislamu kujitokeza kwa wingi kupata faida ya semina hiyo.

 

Amesema semina kama hizo ni muhimu kwa afya ya ndoa, kwani jambo la ndoa ni kubwa na linahitaji kujifunza kama zilivyo taaluma zingine.

 

Naye Khadija Abubakar Amri, Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya kongamno hilo amesema maandalizi yote yako vizuri wanawaomba wananchi kujitokeza ili kupata mafunzo hayo.

 

Faiza Bathigili nae pia amesema kwa sasa Tanzania ndoa nyingi ziko matatizoni na kwamba kuwa uhitaji mkubwa wa jamii kupata elimu zitakazowasaidia kuponya ndoa zao.

 

Amesema kuna baadhi ya nchi ikiwamo Malysia na Zanzibar na indonesia wamefanikiwa kupunguza tatizo la talaka kwa jamii kwa sababu ya uwepo wa semina za na kozi za ndoa ndoa kwa kila mara.

 

Kongamano la wanandoa linatarajiwa kufanyika Jumapili ya Septembea 26, 2021 katika ukumbi wa DYCC uliopo Chang’ombe Jijini Dar es salaam, kiingilio katika semina hiyo ni shilingi 15,000/= kwa mtu mmoja na kwa shilingi 25,000/= kwa watu wawili.

 

Pia Mwenye kiti wa Andalusia KHADIJA ALI ALWY anawakaribisha sana katika kongamano hili na kozi zitapoanza katika vituo husika,na tickets zinapatikana andalusia upanga na k/koo.

Kwa mawasiliano na kwa anaetaka ticket tafadhali wasiliana na ANDALUSIA kwa namba za simu:

 

0784302232/0716561347


Hakuna maoni