Zinazobamba

MBUNGE HALIMA MDEE AKOLEZA MOTO SAKATA LA TUNDU LISSU,AIBUKA NA KUTEMA CHECHE HIZI,SOMA HAPO KUJUA



Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amesema  Chadema kamwe haiwezi kukaa kimya kuhusu tukio la kushabuliwa kwa risasi mbunge wa Singida Mashariki,Tundu Lissu.
 Mbuge wa Kawe, Halima Mdee

Ametoa  kauli  hiyo leo alipokuwa akizungumza na kituo kimoja cha Televisheni nchini, na kwamba wanaodai kuwa chama hicho kimeishiwa sera kwa kulifanya tukio hilo kama agenda  wana hoja nyepesi.

Amasema tukio hilo ni zito ambalo lingeweza kutoa uhai wa kiongozi huyo, hivyo chama kitaendelea kulisema hadi hapo vyombo vya usalama vitakapo chukua hatua stahiki dhidi ya wahusika.

 Amesema jambo kubwa linalowasukuma  kupaza sauti dhidi ya kitendo hicho ni kutokana na Lissu kufanyiwa unyama huo katika eneo ambalo linaaminika liko salama.


Mdee amebainisha  kuwa hawafanyi hivyo  kwa ajili ya kutafuta 'kiki' na kuvitaka vyombo vya usalama kuhakikisha vinawakamata waliofanya shambulio hilo.

"Hatuwezi kukaa kimya kwa matukio yanayotokea, huu siyo utamaduni wetu. Siyo utamaduni wetu watu kupotea bila jeshi la polisi kutoa taarifa inayoeleweka, viongozi kutolewa silaha hadharani na watu ambao wanaaminika wanajulikana lakini hatujaona wakichukuliwa hatua,”

“Mbunge kupigwa risasi maeneo yenye CCTV kamera na waliofanya tukio hilo kutokamatwa, Wananchi kuchanga fedha kwa ajili ya maafa na kisha kutumiwa kwa kazi nyingine na serikali au ni kiki ipi ambayo tunaitumia au kiki ni nini wakati tunakemea mambo yanayohatarisha ulinzi na Usalama?," amehoji Mdee.

Amesema kama ni sera, Chadema bado kina sera  ambazo wanaendelea kuzitekeleza ikiwemo walizoahidi wakati wa uchaguzi na kwamba kama chama hawawezi kushindwa kuwa na sera lakini ni lazima wakemee mambo ambayo awali hayakuwahi kuzoeleka na kuonekana nchini.