Zinazobamba

KUELEKEA KWENYE MTIHANI WA KIDATO CHA NNE KESHO,NECTA WATOA ONYO ILI KALI KWA WANAFUNZI NA WASIMAMIZI WA MTIHANI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Mtihani nchini,Dkt Charles Msonde 
NA KAROLI VINSENT
WAKATI wanafunzi  wa kidato cha nne wakitarajia kuanza kufanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne nchi  kesho,Baraza la Mtihani nchini (NECTA) limesema halitosita kumchukulia    hatua mwanafunzi yeyote pamoja wasimizi wa Mitihani hiyo ambao watajihusisha na vitendo vya udanganyifu kwenye mitihani hiyo .
Pia,Baraza hilo  limewapa onyo wamiliki wa shule kuacha  kuwaingilia wasimamizi wa mitihani hiyo kwakuwa shule zao ni vituo maalum vya kufanyia mtihani.
Onyo hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam,Katibu Mtendaji wa (NECTA),Dkt Charles Msonde wakati wa mkutano na waandishi,amesema Baraza hilo linatoa wito kwa  kwa wasimamizi wa mitihani  wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu.
“Tunawaasa wasimamizi wa mitihani pamoja na wanafunzi kujiepesha na vitendo vya udanganyifu  kwani Baraza  litachukua  hatua kali kwa yeyote  yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya Taifa”Amesema Dkt Msonde.

Amesema Baraza hilo linawataka  wamiliki wa shule kutambua  kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani  na hivyo havitakiwi kuingilia majukumu ya wasimamizi.
“Baraza halitasita kukifuta kituo  chochote cha Mitihani endapo litajiridhisha kuwa uwepo wake wa unahatarisha Usalama wa Mitihani ya Taifa”amesema Dkt Msonde.

Hata hivyo,Dkt amesema Baraza hilo linaamini  kuwa walimu wamewaandaa vizuri wanafunzi hao kwa kipindi cha miaka mine ya elimu ya sekondari hivyo hakutakuwepo na vitendo vya udanganyifu.
Pamoja na hayo,Amesema katika mitihani huo Jumla ya watahiniwa 585,938 wamesajiliwa kufanya mtihani wa huo, ambapo kati yao watahiniwa wa shule ni 323,513 na watahiniwa wa kutegemea ni 62,425.
“Kati ya watahiniwa wa shule 323,513 waliosajiliwa ,wanaume ni 159.103 sawa na asilimia  49.18 na wanawake  ni 164,410 sawa na asilimia 50.82,huku watahiniwa wenye uono hafifu ni 305 ambapo maandishi yao yanakuzwa”amesema Dkt Msonde.
Kuhusu watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa ni 62,425 ,wanaume ni 28,574 sawa na asilimia 45.77  na wanawake ni 33,851 sawa na asilimia 54.23 huku watahiniwa 6 wasioona.


Aidha,Baraza hilo linatoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano katika kuhakikisha mitihani hiyo ambayo inaanza kesho octoba 30 hadi 17  Novemba 2017 inafanyika kwa Amani na Utulivu huku akiwaomba wananchi hao kuheshemu eneo la mtihani linapofanyika.