Zinazobamba

WAKENYA MILIONI 19 KUAMUA HATMA YA NCHI YAO LEO,SOMA HAPO KUJUA

Wakenya milioni 19 wanashiriki kwenye uchaguzi wa kihistoria leo

Kiongozi wa chama tawala cha Jubilee, Rais Uhuru Kenyatta, anachuana tena na hasimu wake wa kisiasa, Raila Odinga wa muungano mkuu wa upinzani, NASA, kwenye kinyang'anyiro kinachotazamiwa kuwa cha vuta ni kuvute baina ya wawili hao, licha ya kuwepo wagombea wengine saba wa urais.

Uchaguzi huo unaowagharimu walipakodi wa Kenya shilingi bilioni 49 unaelezwa kuwa ghali zaidi ikilinganishwa na uchaguzi katika mataifa jirani.

Zaidi ya wagombea 1,000 watachaguliwa na Wakenya kwenye nafasi za urais, ugavana, useneta, ubunge, uwakilishi wa akinamama na wa kaunti mbalimbali.

Kuna vituo elfu 40,883 vya kupigia kura vitakavyolindwa na maafisa 150,000 wa idara za usalama, na zaidi ya waangalizi 9,000 wa kitaifa na wa kigeni wameidhinishwa kuangalia uchaguzi huu.