Zinazobamba

SERIKALI YA MAGUFULI YAKOMALIA POMBE ZA VIROBA,YAIBUKA NA HILI LEO,SOMA HAPO KUJUA


Serikali imefuta usajili na utoaji vibali vya uzalishaji, uingizwaji, usambazaji na uuzwaji wa pombe kali iliyofungashwa katika karatasi maarufu kiroba, na pombe zilizofungashwa katika chupa ndogo zenye ujazo chini ya mililita 200 kuanzia Machi Mosi, mwaka huu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema hayo Dar es Salaam leo katika Mkutano wake na waandishi wa habari.

"Kwa viroba ambavyo tumevikamata tunasubiri maelekezo toka ofisi ya waziri mkuu iwapo viharibiwe au virudishwe viwandani vikafungashwe katika vifungashio vinavyokubalika kitaifa