RIDHIWANI KIKWETE ASEMA HAYA BAADA YA MAMA YAKE KUTEULIWA UBUNGE,SOMA HAPO KUJUA
Mbunge wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani Ridhiwan
Kikwete amefunguka baada ya mama yake jana kuteuliwa na Rais Magufili kuwa
Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ridhiwan Kikwete amesema kuwa mama Salma Kikwete ni
mwanamke wa shoka kwani amewezesha wasichana wengi nchini Tanzania kupata elimu
na amekuwa mtetezi wa haki za wanawake hivyo anaamini kupata nafasi ya kuwa
Mbunge itakwenda kuwezesha mapambano kuwa sheria rasmi.
"Umekuwa mtetezi wa haki za
wanawake na usawa wa kijinsia, umewezesha wasichana kupata elimu. Wewe ni
mwanamke wa Shoka. Hongera sana kwa uteuzi. Imani sasa umepata sehemu ya
kuwezesha mapambano kuwa sheria. Mungu akutangulie Mama yangu , Mheshimiwa
Mbunge. Hongera tena" aliandika Mhe. Ridhiwan Kikwete