DC HAPI AIKATAA BENKI YA DCB KINONDONI,SOMA HAPO KUJUA
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi akizungumza na watendaji mbali mbali wakati akiwa kwenye ziara yake ya siku kumi kwenye kata zote zilizopo kwenye manispaa yake ,lengo la ziara yake hiyo ni kukagua miradi ya maendeleo ya serikali pamoja na kusikiliza kero za wananchi, |
NA KAROLI
VINSENT
Mkuu wa
wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi ameiagiza manispaa hiyo kutafuta mfumo wa mpya na
rafiki ambao utaweza kuwakopesha fedha wamama na vijana, ili kuachana na mfumo
wa sasa wa kutumia Benki ya DCB kutoa
mikopo hiyo ambao umetajwa kugubikwa na urasimu mwingi.
Hapi ambaye
ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa wilaya hiyo,ametoa agizo hilo Leo wakati
alipokuwa kwenye ziara katika kata ya Mbezi juu ikiwa ni mwendelezo wa ziara
yake ya siku 10 katika kata zote zilizopo wilaya ya Kinondoni,ziara hiyo yenye
lengo la kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kusikiliza kero za
wananchi.
Amewataka Watendaji hao, watafute mfumo rafiki na mzuri ambao utakaotumika katoa mikopo kwa walengwa.
Amewataka Watendaji hao, watafute mfumo rafiki na mzuri ambao utakaotumika katoa mikopo kwa walengwa.
"Tafuteni mfumo ambao kila mhusika ikiwemo vikundi anayetaka mkopo kutoka kwenye Halmashauri apate mikopo hii bila upendeleo,na mfumo huo usaidia kukusanya marejesho bila ya kuweka riba yeyote " Ameelekeza Hapi.
Hapi
amebainisha kuwa mfumo wa sasa wa kuwakopesha mikopo vijana kutumia Benki ya
DCB umekuwa na Mazingira yasiokuwa rafiki na kupelekea vijana wengi kushindwa
kupata mikopo hiyo.
"Yaani
Benki hii Leo hata ukienda kuwaambia wakupe mrejesho wa fedha walizochukua za
halmashauri kwa ajili ya kuwakopesha Mikopo watu wanakwambia hawana,yaani wanachukua fedha
za halmashauri wanafanyia biashara kinyume na lengo letu La kutoa mikopo bila
riba'" amesema Hapi.
Amedai kuwa
urasimu huo ndani ya Benki hiyo umechangia walengwa wengi kushindwa kunufaika
na mikopo hiyo jambo analodai hatalikubali.
Katika hatua
nyingine,Hapi amewataka watendaji wa kata ya Mbezi juu kuacha kasumba ya
kuitegemea serikali kila kitu badala yake amewataka kuwa wabunifu katika
kautatua matatizo katika maeneo yao.
"Kama
kila kitu mnategemea serikali kila jambo hamtofika,kuweni wabunifu jamani,Leo
tafuteni wadau wa Maendeleo mchangishane mpate fedha kwa ajili ya Ujenzi wa
madarasa,sio kila kitu serikali kama mkiwa hivyo hamtafika" amesema Hapi,
Hapi pia
katika ziara hiyo amekagua Ujenzi wa shule,na baadae akasikiliza kero za
wananchi.