Zinazobamba

DC HAPI AWAONYA WATENDAJI KINONDONI,SOMA HAPO KUJUA


NA KAROLI VINSENT
WATENDAJI na viongozi wa Manispaa ya Kinondoni wametakiwa kujiepusha na ukusanyaji wa fedha za wananchi bila kupata kibali cha Mkurugenzi wa manispaa ili kuepusha migongano na ufujaji wa fedha za wananchi.
Aidha, wametakiwa kuhakikisha wanatoa risiti za mashine za kielektroniki (EFD) kwa kila michango halali wanayokusanya ili kupunguza malalamiko ya wananchi kutopewa risiti wanapotoa michango.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi wakati akiwa kwenye Kata ya Makongo Juu ambako alitembelea kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero mbalimbaki za wananchi.
Hapi alisema kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakikusanya fedha bila utaratibu kutoka kwa wananchi na kuzitumia kinyume na utaratibu hali ambayo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo.
"Kama viongozi mnataka kukusanya fedha za wananchi ni vema mkaomba kibali ili yakitokea malalamiko tujuee yanatoka wapi na tunayashughulikia vipi. Huko nilikopita nimekutana na kesi hizo wanakusanya michango, lakini haifiki," alisema Hapi.
Alisema zipo kesi kadhaa za viongozi kutumia fedha za wananchi na hasa Wenyrviti wa serikali za mitaa na baadhi yao wamekuwa wakiweka fedha hizo kwenye akaunti zao binafsi badalaya ya akaunti za mitaa yao.
"Kama wananchi wanataka kuchangia, waelekezeni utaratibu mzuri ambao hakutakuwa na malalamiko alkini pia na nyinyi msije mkaingia doa kwenye uongozi wenu," alisema.
Katika hatua nyingine, Hapi alitoa siku tatu kwa Kamati za Maendeleo za mitaa kuhakikisha zimebandika taarifa za mapato namatumizi ya mitaa yao katika mbao za matangazo ili kuweka uwazi.
Alisema kamati hizo zina wajibu wa kuwasomea wananchi wao taarifa za mapato na matumizi.
Hapi pia alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imepiga marufuku kutoa michango ya aina yoyote, hivyo ikibainika wapo wakuu wa shuke ambao wanaenda kinyume na agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria