Zinazobamba

ACT WAZALENDO WAENDELEA KUMKUMBUSHA RAIS MAGUFULI,KUHUSU KATIBA MPYA,SOMA HAPO KUJUA



 
Naibu Katibu Mkuu ACT-Wazalendo, Msafiri Mtemelo amesema wananchi wanapaswa kupiga kelele kuhusu mkwamo wa Katiba Mpya kwani serikali ilitumia mabilioni katika mchakato huo.

Akizungumza katika mkutano Mkuu wa kitaifa wa Katiba ulioandaliwa na Jukwaa la Katiba leo, Mtemelo alisema   wananchi wanapaswa  kulipigia kelele suala la katiba kwani nguvu kubwa imetumika kwa kuunda Bunge la Katiba na wawakilishi kuzunguka nchi nzima kukusanya maoni lakini imeachwa bila kumalizwa.

"Lazima serikali iliyopo madarakani itambue kwamba katiba ni maridhiano kati ya mtawala na mtawaliwa, lakini katiba zote zilizopitishwa toka mwaka 1961 mpaka leo, hakuna ambayo wananchi walihusishwa bali kumekuwa na kundi dogo la watu na wanasiasa ambao ndiyo wanatumika na siyo wawakilishi wa wananchi," alisema Mtemelo.