JUKKWAA LA KATIBA WAMUOMBA MAGUFULI KUTANGAZA TAREHE YA MCHAKATO WA KATIBA MPYA...WASEMA WAKATI NI SASA
NA MWANDISHI WETU
JUKWAA
la Katiba Tanzania(JUKATA) wamemtaka rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutangaza tarehe rasmi
ya kuendelea kwa mchakato wa kupata katiba mpya ya Tanzania.
Endapo
jambo hilo haliatekelzwa basi wataangalia namna nyingine ikiwemo
kuhamasisha wabunge ili kulizungumzia jambo hilo katika bunge lilalo kwa
kumuuliza Waziri Mkuu ili aiwezekan kuweka bayana kama mchakato huo
utarudishwa kuanzia lini na utaanza na kipengele kipi.
Akizungumza
wakati wa Mkutano Mkuu wa Kitaifa waJukwaa hilo, Mwenyekiti wa JUKATA,
Deus Kibamba alisema kuwa wameamua kuja na tamko hilo la kumtaka Rais
kutangaza tarehe hiyo kutokana na kutoridhishwa na utendaji wake kwa
kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja toka aingie madarakani.
Alisema,
wao kama jukwaa hawakutarajia kama hadi sasa serikali ingeweza kukaa
kimya juu ya suala hilo kwani matarajio ya wengi ilikua kuona zoezi hilo
lipo katika mipango ya utekelezaji wake.
Alisema
kuwa ndoto yao kubwa ilikuwa kuona kuwa jambo hilo Linatekelezwa kama
ilivyoahidiwa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika
miaka mwaka 2015.
Alisema
katika kipindi cha kampeni ilani za uchaguzi za Chama cha Mapinduzi,
Chama cha Demokrasia na Mwendelezo CHADEMA pamoja na ACT wazalendo
zilikuwa zikizungumzia kutoa kipaumbele kwa mchakato huo.
Kibamba
alisema kuwa, qa sasa wanashindwa kuelewa kwanini viongozi hao ikiwemo
wabunge hawaweki suala hilo hata katika dondoo za vikao vyao vya ndani
toka walipopewa madaraka na wananchi ya kuwawakilisha bungeni.
Alisema, atashangaa sana endapo hatoona Waziri wa Katiba na Sheria____hatotenga bajeti katika bunge litakloanza mwezi Aprili
La bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa jambo hilo.
"Kipindi
cha kampeni ahadi za kuendelea mchakato huu zilokuwa nyingi lakini toka
viongozi hao wapungue madarakani hakuna jambo lolote linalofanyika
kuonesha kufikia mkazo suala hilo" alisema Kibamba.
Alisema
kuwa jambo linalokatisha tamaa zaidi ni kauli za rais za kudai kuwa
Hajawahi kutoa ahadi yoyote kuhusiana na kuendelea mchakato qa
kupatikana kwa katiba mpya.
"Kauli
ya rais ya kusema kuwa hajawahi kutoa ahadi hiyo inawachanganya
watanzania wengi kwani rasmi zao zinaonesh kuwa nchi kupata katiba mpya
ni moja ya ajenda zilizokuwa zikizungumziwa sana na viongozi ni
kupatikana wa katiba mpya.
Kwa upande wake mbuge wa Jimbo la Ubungo wa tiketi ya CHADEMA, Said Kubenea alisema kuwa
Mchakato
huo unapaswa kuanzia pale ilipoishia tume ya jaji mstaafu Sinde Warioba
kwa kuunda bunge na kupitiwa tena na mamlaka za kisheria ambavyo
yatazingatia kuboresha maoni yaliyokusanywa na tume ya maoni ya katiba
na si kunyofoa mambo muhimu kama ilivyofanywa katika rasimu ya katiba
iliyopendekezwa.
Alisema
katika mapendekezo vitu vya muhimu vilivyotolewa ni mfumo wa Serikali
tatu, upahikanaji wa wabunge pamoja na uendeshaji wa nchi jambo
linalofanya rasimu hiyo isifae kupigiwa kura.
"Leo
tunona kuna teuzi za wabunge 10 wa rais, kwa maoni yangu nafasi hizo
zingewekwa kumsaidia rais kuteua watu watakaomsaidia kuunda Serikali
kama ataona ndani ya bunge hakuna wataalamu mfano kuhusiana na mmbo ya
majeshi au mmbo mengine na si kufanya nafasi hizo kama dadake", alisema
Kubenea.
Alisema
kuwa kwa maoni yake anaona ucheleweshwaji wa katiba hiyo hauna athari
sana kwani haraka huenda ikapelekea wananchi kupata katiba yenye
mapungufuna isiyokidhi matakwa ya wengi zaidi ya hii inayotumika sasa ya
mwaka 1977.
"Endapo
tutataka katiba hii ipatikane haraka basi huenda tunaingia katika
machafuko au kupata katiba yenye mapungufuna mengi kwani rasimu hii
imetengenezwa na wabunge wa upande mmoja bila kushirikisha upande wa
upinzani ambao kwa kiasi kikubwa walikua wanaunga mkonotume ya jaji
Warioba" alisema Kubenea.