ASKOFU GWAJIMA SAKATA LAKE LAUMIZA KICHWA JESHI LA POLISI,SOMA HAPO KUJUA
Wakili Peter Kibatala amesema polisi wamepiga picha nyumbani kwa Askofu
wa Kanisa la Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat
Gwajima.
Kibatala ambaye ni wakili wa Askofu Gwajima amesema jana kuwa mbali na
kupekuwa na kupiga picha kila kona walikwenda katika kanisa lake
lililopo Ubungo.
“Waache wafanye yao na sisi tutafanya yetu kisheria. Kwani hatuwezi
kuwazuia Polisi kufanya shughuli yao na baada ya kumaliza na sisi
tutajua nini cha kufanya,” amesema Kibatala.
Msemaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, David Mngongolwa amesema Gwajima alikwenda jana kuripoti kama alivyoamriwa kufanya hivyo.
Mngongolwa amesema baada ya kuripoti askari walimchukua na kwenda naye
nyumbani kwake wakakaa kwa dakika zisizozidi sita na kuondoka naye.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda amesema hana
taarifa za kukamatwa kwa Gwajima kwa maelezo kuwa alikuwa katika kikao.
“Naomba uumtafute Sirro (Simoni-Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar
es Salaam. Gwajima awali alishikiliwa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es
Salaam hivyo ni vema ukamtafuta kamishna,” amesema Kamanda Kaganda.