ZITTO KABWE AMPA MASHARTI MAGUMU RAIS MAGUFULI,SOMA HAPO KUJUA

Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amemshauri Rais
wa Tanzania Dkt. John Magufuli kulivunja Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania endapo analiona ni kikwazo kwake.
Ushauri huo ameutoa jana ikiwa ni saa chache baada
ya Rais Magufuli kukosoa uamuzi wa Bunge kumuita Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Paul Makonda kujieleza mbele ya Kamati ya Bunge, kutokana na kilichodaiwa na
wabunge kuwa ni kauli ya kulidhalilisha Bunge.
Katika hotuba yake aliyoitoa jana wakati wa
kuapishwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za
Kulevya, Rais Magufuli aliwataka viongozi wengine kumuunga mkono mtu
anayejitokeza kupiga vita dawa za kulevya badala ya kumdhalilisha.
"Tunapomuona mtu anajitokeza
kupambana na haya madawa ya kulevya, badala ya kumdhalilisha tumuombee na
kumtia moyo, hawa wanaweza hata kubadilisha maneno uliyoyazungumza
wakabadilisha wakatengeneza kwenye clip wakatupa, na wakajitokeza wengine
wakasema wameingilia mamlaka yao, wakati wao wanaingilia mamlaka ya kuwaita
wengine, hii ni vita". Alisema Magufuli
Baada ya kauli hiyo ya Rais, Zitto kupitia ukurasa
wake wa Facebook ameonesha kushangazwa na kile alichodai kuwa Rais
hakujua kuwa sheria ya kuundwa kwa mamlaka hiyo, ilitungwa, na kwamba
anashangaa kuona Rais hakuwa akijua kuwa alipaswa kumteua Kamishna Mkuu wa
Mamlaka hiyo
Ujumbe wa Zitto unasema
"Wabunge walitoa Hoja Binafsi
kuhusu Madawa ya kulevya ( Esther Bulaya na Faustine Ndugulile ) na kufuatia
hoja hiyo Serikali ikaleta Muswada bungeni na Bunge likatunga Sheria ya Kupambana
na Madawa ya kulevya mwaka 2015.
"Serikali mpya ikaingia madarakani
mwezi Novemba 2015. February 2017 Ndio Kamishna Mkuu anateuliwa tena baada ya
wabunge kuhoji na kushinikiza kupitia Kamati husika na pia mbunge Esther Bulaya
aliyetoa Hoja Binafsi katika Bunge la Kumi.
"Rais anasema hakuwa anajua kuwa
sheria hiyo ipo. Lakini Rais anapogawa Wizara huwa anatoa instruments na Hizo
instruments hutaja kila sheria kwa kila Waziri. Ilikuwaje Rais akasahau sheria
hii nyeti kama alikuwa na nia ya dhati ya Kupambana na Madawa ya kulevya?
Rais anaona Bunge kikwazo kwa sababu
Bunge linamwongoza afuate sheria. Lakini Kama anaona Bunge linamkera turudi
kwenye uchaguzi tu, alivunje".