TID AWAOMBA RADHI WATANZANIA KWA UTUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA,AKIRI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA

Msanii wa Bongo fleva Khalid Mohamed (TID) amesema
kuwa hawezi kufumbia macho wala kuwaonea
aibu kwa kuwataja watu wote ambao wanafanya biashara ya dawa za kulevya.
TID amesema hayo jijini Dar es Salaam katika mkutano
wa mkuu wa mkoa na waandishi wa habari juu ya mapmbano dhidi ya dawa za kulevya
kwa mara ya tatu.
“Mimi mnyama na mkuu wa mkoa kaonesha unyama katika kupambana na madawa ya kulevya, hivyo namshukuru sana kwa hatua ngumu aliyoamua kuichukua,basi wote kwa pamoja tuanze kupambana na kuhakikisha biasha hii inapungua kama sio kuisha kabisa,tushiriki kwa pamoja kukomesha biashara hii kwa kupinga janga hili ” amesema TID.
TID ambaye amekiri hadharani kuwa amekuwa akitumia dawa za kulevya kwa muda mrefu lakini zimekuwa zikimtesa ,hivyo RC Makonda amekuwa msaada kwake,
“Mimi mnyama na mkuu wa mkoa kaonesha unyama katika kupambana na madawa ya kulevya, hivyo namshukuru sana kwa hatua ngumu aliyoamua kuichukua,basi wote kwa pamoja tuanze kupambana na kuhakikisha biasha hii inapungua kama sio kuisha kabisa,tushiriki kwa pamoja kukomesha biashara hii kwa kupinga janga hili ” amesema TID.
TID ambaye amekiri hadharani kuwa amekuwa akitumia dawa za kulevya kwa muda mrefu lakini zimekuwa zikimtesa ,hivyo RC Makonda amekuwa msaada kwake,
Akasema na kuongeza
kuwa hahitaji nguvu ya dola kuacha uvutaji wa dawa za kulevya,hivyo ameamua kuacha mwenyewe ili awe mfano wa
kuigwa .
Amesema yeye bado ni kijana hana kasoro yoyote wala ulemavu wowote,hivyo itakuwa ni aibu kwake kuonekana mtumiaji wa dawa za kulevya mbele ya mtoto wake, hivyo atakuwa hajengi familia bali atakuwa anaibomoa kwa kumfanya mtoto aendelee kuiga tabia mbovu za baba yake.
Amesema yeye bado ni kijana hana kasoro yoyote wala ulemavu wowote,hivyo itakuwa ni aibu kwake kuonekana mtumiaji wa dawa za kulevya mbele ya mtoto wake, hivyo atakuwa hajengi familia bali atakuwa anaibomoa kwa kumfanya mtoto aendelee kuiga tabia mbovu za baba yake.