KESI YA MSANII WEMA YAAHIRISHWA,MASOGANGE NAYE PANDISHWA MAHAKAMANI,SOMA HAPO KUJUA
Mwigizaji Wema Sepetu leo alienda tena
Mahakamani baada ya kuachiwa kwa dhamana kwenye sakata la dawa za kulevya baada
ya kutajwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi 15 March 2017
baada ya upande wa Mashtaka kusema upelelezi bado haujakamilika
NAYE
MREMBO WA VIDEO MASOGANGE KESI YAKE YAWA HIVI.
Msanii
Agnes Gerald 'Masogange' amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka ya kutumia dawa za kulevya.
Mrembo
huyo ambaye ni maarufu kwa kupamba video za muziki wa wasanii wa bongo fleva,
amekana tuhuma hizo na kesi yake kuahirishwa hadi Machi 2i mwaka huu.
Katika
mashtaka yake mawili yaliyosomwa na mwendesha mashtaka Mashauri Wilboard chini
ya wakili wa serikali Constatine Kokulwa, Agnes anadaiwa kutumia dawa za
kulevya aina ya Heroin na Oxazepan kwa nyakati tofauti.
Mara baada
ya kusomewa mashtaka yake, ameachiwa kwa dhamana ya wadhamini wawili pamoja na
kusaini bondi ya shilingi milioni 10.
Pia mrembo
huyo ambaye amewahi kukamatwa nchini Afrika Kusini akihusishwa na usafirishaji
wa dawa za kulevya, ametakiwa kutotoka nje ya Dar es Salaam kwa kipindi chote
cha kesi bila kibali cha mahakama.