Zinazobamba

CCM YANGUKIA PUA KESI YA UBUNGE,SOMA HAPO KUJUA



CC
Mahakama ya Rufani Kanda ya Arusha leo imetupilia mbali rufani ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Longido Onesmo Ole Nangole (Chadema), baada ya kukiuka amri ya Mahakama hiyo iliyomtaka afanye marekebisho kwa kuandika upya rufani yake.

Akisoma uamuzi wa Mahakama, Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Amir Msumi, amesema, Ole Nagole alikiuka amri ya Mahakama iliyotolewa Oktoba 24, mwaka jana iliyomtaka aongeze majina ya Msimamizi wa Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika rufani yake mpya kabla ya kesi kusikilizwa..

Mh. Jaji Msumi amesema Mahakama imeridhishwa na pingamizi lililowasilishwa na upande wa Mjibu Rufani, Dk. Masumbuko Lamwai, (CCM), aliyetaka rufani hiyo isisikilizwe kwa madai imeandikwa upya bila idhini ya Mahakama.

Matokeo ya Ubunge wa Onesmo Ole Nangole yalitenguliwa Juni 29 mwaka jana, kwa madai kulikuwa na dosari nyingi ikiwemo kujazwa matokeo ya Ubunge kwa kutumia fomu namba 21c za kujaza matokeo ya udiwani na kujaza matokeo ya Ubunge, badala ya kutumia fomu namba 21b.

Ole Nangole alikuwa akipinga kutenguliwa kwa matokeo hayo ambapo alikuwa akipambana na mgombea wa CCM Dk, Steven Kiruswa