TRA YAZINDUA MPANGO KAPAMBE,NI WA KUBORESHA TAARIFA ZA MLIPA KODI,SOMA HAPO KUJUA
![]() |
| Pichani ni
Kamishna
wa TRA Bw. Alphayo Kidata akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za
TRA jengo la Milenium Makumbusho leo wakati akielezea kampeni ya kuhakiki namba
ya utambulisho wa mlipa kodi TIN itakayoendelea mpaka mwezi wa kumi mwaka huu
nchini kote, kulia ni Kamishna wa Kodi za Ndani Bw.Elaijah Mwandumbya.
|
MAMLAKA
ya Mapato nchini (TRA) kupitia kwa Kamishina Mkuu wa Ofisi hiyo wamezindua
zoezi maalumu kwaajili ya kuhakiki na kuboresha taarifa za usajili
wa namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN) .
Uzinduzi
huo umefanywa na Kamishna Mkuu wa Ofisi hiyo , Alphayo Kidata kwa kushirikiana
na wafanyakazi wa ofisi hiyo mapema hii leo jijini Dar es salaam, hivyo kuanzia
sasa zoezi hilo litakuwa endelevu katika mikoa yote nchini ya bara na visiwani ,
Kidata
alisema kuwa lengo kubwa la uzinduzi wa zoezi hilo ni kubadili mfumo wa sasa wa
kuhifadhi kumbukumbu za walipa kodi kwa kuweka mfumo mpya unaoendana na ukuaji
wa teknolojia ambao utakuwa na walipa kodi wake wanaostahili kuwepo
kwenye wigo.
Aidha
aliongeza kuwa mfumo huo utasaidia kuwaondoa walipa kodi hewa ,kuongeza
ufanisi katika suala zima la usimamizi wa ukusanyaji kodi kwa
kiwango cha juu na kuwezesha ulipaji kodi kuwa nafuu kwa mlipaji.
Hata
hivyo katika hatua nyingine Kidata ametoa wito kwa yeyote mwenye namba ya
utambulisho wa mlipa kodi kufika katika ofisi za mamlaka hiyo ili kuweza
kupata utaratibu wa zoezi zima jinsi linavyokwenda
