MFUMO WA ELIMU WA SASA UBADILISHWE,RODRIGUZ WA UN ATOA USHAURI WA SERIKALI YA JPM,SOMA HAPO KUJUA
| Pichani nI Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwa upande wa Tanzania Alvaro Rodriguz (picha na Maktaba) |
NA KAROLI VINSENT
SERIKALI nchini imetakiwa kubadilisha mfumo wa elimu
ya sasa ambao umebainika unamwandaa mhitimu kutegemea ajira na kwenda kwenye mfumo wa elimu unaomwandaa
mhitimu kujitengenezea ajira na kuwa mbunifu.
Imeelezwa njia hiyo italisadia taifa ambapo katika
kipindi hichi cha serikali ikitarajia
kuwekeza zaidi kwenye Viwanda..
Ushauri huo umetolewa na Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwa upande wa Tanzania Alvaro Rodriguz wakati wa Mkutano na
Waandishi wa habari wenye lengo la kumwaga Mwakilishi mkazi wa umoja wa Taifa ambalo
linashughulikia idadi ya watu UNFPA, Dr Natalia Kanen ambaye amechanguliwa kuwa
Naibu Katibu mkuu kwa upande wa Dunia
,
Rodriguz amesema kwa sasa Tanzania kila mwaka vyuo
vyake inazalisha wasomi wanaomaliza Chuo kikuu wanaofikia milioni 1 huku wengi
wao wakikosa ajira.
Amesema Njia sahihi ya kuweza kuwasaidia watu hao ni
kwa serikali kubidilisha mfumo wa elimu wa sasa na kuupeleka kwenye mfumo wa
elimu utakaoweza kuwajengea wahitimu kuwa wabunifu.
Kwa Upande wake,Naibu Katibu mkuu mpya,Dr Kanen
amewapongeza viongozi wa Tanzania kwa kufanya nae kazi kwa ushirikiano kwa
zaidi ya miaka miwili aliyokuwa hapa nchini.
Amesema Ushirikiano aliopata hapa Tanzania
umepelekea hadi kuchaguliwa kushika nafasi.huku akiwahasa Watanzania
kuhakikisha wanamuinia mtoto wa kike kwa kumpatia elimu ambayo amedai itaweza
kumkomboa na kulileta taifa maendeleo.