MAGUFULI ATUMBUA JIBU HILI LEO,SOMA HAPO KUJUA

FALSAFA ya Rais John Magufuli ‘tumbua jipu’
inaendelea ambapo leo, amemtubua Prof. William Lyakurwa, aliyekuwa Mwenyekiti
wa Benki ya Maendeleo ya TIB, anaandika Hamisi Mguta.
Taarifa iliyotolewa na Gerson
Msigwa, Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa, Rais
Magufuli amemteua Prof. Palamagamba Kabudi kuchukua nafasi hiyo.
Taarifa
hiyo imeeleza kwamba Prof. Lyakurwa aliyekuwa mwenyekiti katika bodi hiyo kwa
miaka mitatu.
“…
ametenguliwa kutokana na mamlaka aliyonayo rais chini ya kifungu cha 48 cha
sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act),” imeeleza taarifa
hiyo.
Kutokana
na mabadiliko hayo Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango ametengua
uteuzi wa wajumbe wa benki hiyo.
“Dk.
Mpango, kutokana na mamlaka aliyonayo kupitia kifungu cha 9 (1) cha sheria ya
mashirika ya Umma amewateua Brigedia
Generali Mabula Mashauri, Dk. Razack B.
Lokina, Bi. Rose Aiko, Prof. Joseph Bwechweshaija, Said Seif Mzee, Dk. Arnold
Kihaule, Maduka Paul Kessy, Charles Singili kuwa wajumbe wapya wa bodi hiyo
kuanzia leo,” imeeleza taarifa hiyo.
Post Comment
Hakuna maoni
Chapisha Maoni