TRA YAZIDI VUNJA REKODI YA MAPATO NCHINI,YATIA FORA KWA MWENZI MACHI,SOMA HAPO KUJUA
| Pichani ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA),Alphayo Kidata akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam |
MAMLAKA ya
Mapato nchini (TRA) imezidi vunja rekodi ya ukusanyani wa mapato baada ya
kukusanya mapato ya zaidi ya trioni 1.316 ambayo ni sawa
na asilimia 101.0 kwa mwezi Machi ikiwa ni kiwango kikubwa tofauti na malengo
waliyojiwekea ya kukusanya trioni 1.302 kwa mwezi huo.Anaaandika KAROLI VINSEN
endelea nayo
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Kamishna
mkuu wa TRA,Alphayo Kidata wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo
amesema hali ya ukusanyaji wa kodi nchini inaendelea vizuri kwa madai kuwa TRA
inavuka malengo ya ukusanyaji kodi waliyojiwekea.
“Tunazidi vunja rekidi ya ukusanyaji wa mapato kwani
kwa mwezi Machi tulijiwekea malengo ya kukusanya Trioni 1.302 lakini baada
kuweka mipango dhabiti tumejikuta tumekusanya Trioni 1.316 ambayo ni sawa na
asilimia 101.0”amesema Kidata.
Kidata, ametoa sababu zilizopelekea TRA kuzidisha
kiwango hicho cha ukusanyaji wa kodi imetokana na kuongezeka kwa kasi ya usimamizi,ufuatiliaji
na ukadiriaji wa kodi kwa usahihi na bila uonevu pamoja na kudhibiti biashara
za magendo katika maeneo ya ukanda wa Pwani wa bahari ya Hindi pamoja na mipaka yote ya nchi.
Pamoja na hayo,Kidata ametoa wito kwa
wafanyabiashara wote nchini ambao hawajasajili biashara zao kufanya hivyo mara
moja kupitia ofisi za TRA zilizopo katika maeneo yao.
Katika Hatua nyengine,TRA imesema inajaandaa kutoa
mashine za kielekroniki za Kodi (EFDs) bure kwa wafanyabiashara nchini ikiwa ni
kutii agizo la Rais John Magufuli aliitoa kwa Mamlaka hiyo kutoa mashine hizo
bure.
No comments
Post a Comment